1Nyuma ya Sanduku la Yawe kukaa katika inchi ya Wafilistini kwa muda wa miezi saba,
2Wafilistini waliwaita makuhani na waaguzi wao na kuwauliza: “Tufanye nini na Sanduku hili la Yawe? Mutuambie namna gani tunavyoweza kulirudisha kwa nafasi yake.”
3Wao wakawaambia: “Mukirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, musilirudishe mikono mitupu. Lakini munapolirudisha mupeleke na sadaka ya malipo ya kosa kwa kuondoa makosa yenu. Mukifanya hivyo mutapona, nanyi mutafahamu kwa nini amekuwa akiwaazibu kwa mufululizo.”
4Watu wakauliza: “Tutamutolea nini kwa malipo ya makosa?” Wao wakawajibu: “Sanamu tano za zahabu mufano wa majipu, na sanamu tano za zahabu mufano wa panya, kufuatana na hesabu ya wakubwa wa Wafilistini, maana kulikuwa pigo moja tu, kwa ninyi wote na kwa wakubwa wenu.
5Basi mufanye sanamu zenu za majipu na sanamu za panya, vitu ambavyo vinaangamiza inchi yenu, nanyi mutamutukuza Mungu wa Israeli. Labda ataacha kuwaazibu ninyi wenyewe, miungu yenu na inchi yenu.
6Kwa nini munafanya mioyo yenu kuwa migumu kama Wamisri na Mufalme wao? Mungu alipowachekelea Wamisri, hawakuwaacha Waisraeli waondoke, nao wakaondoka?
7Basi, mutayarishe gari jipya na ngombe wawili wenye kunyonyesha ambao bado hawajafungwa nira. Muwafunge kwenye gari hilo lakini vitoto vyao visiende pamoja nao, lakini vibaki katika zizi.
8Mutwae Sanduku la Yawe na kuliweka katika gari hilo. Muweke zile sanamu za zahabu ambazo munamupelekea kama sadaka ya malipo ya makosa yenu pembeni ya Sanduku. Kisha muliache liende litakakokwenda.
9Lakini muangalie. Ikiwa gari hilo linakwenda moja kwa moja kuelekea inchi yake, ni kusema kwenye muji wa Beti-Semesi, basi, pale tutajua kwamba aliyetuletea pigo hili ni Mungu wa Israeli. Lakini kama haliendi kule, basi, tutajua kwamba sio mukono wake uliotupiga, lakini hasara hii imetupata kwa bahati mbaya.”
10Walifanya kama walivyoambiwa; walitwaa ngombe wawili wenye kunyonyesha na kuwafunga kwenye gari, na vitoto vyao wakavifunga katika zizi.
11Lile Sanduku la Yawe wakalitia kwenye gari hilo pamoja na kile kibweta chenye kuwa na sanamu za zahabu za panya na zile za majipu.
12Wale ngombe walikwenda moja kwa moja kuelekea muji wa Beti-Semesi bila kupinda kushoto au kuume, walikuwa wanalia walipokuwa wanakwenda. Wale wafalme watano wa Wafilistini waliwafuata mpaka kwenye mupaka wa Beti-Semesi.
13Watu wa Beti-Semesi walikuwa wanavuna ngano katika bonde. Walipoangalia juu na kuliona Sanduku la Yawe, wakafurahi sana.
14Hilo gari lilielekea kwenye shamba la Yoshua, mukaaji wa Beti-Semesi. Lilipofika hapo likasimama karibu na jiwe kubwa. Watu wakalibomoa lile gari, wakatumia mbao zake kwa kuwateketeza hao ngombe ambao waliwatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.
15Walawi walikuwa wameliteremusha Sanduku la Yawe na kile kibweta chenye sanamu za zahabu na kuziweka kwenye lile jiwe kubwa. Basi, siku hiyo watu wa Beti-Semesi walitoa sadaka za kuteketezwa, na kumutolea Yawe sadaka.
16Wale wakubwa watano wa Wafilistini walipoona hayo, walirudi Ekuroni, siku ileile.
17Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.
18Walipeleka vilevile sanamu za zahabu za panya kulingana na hesabu ya miji yote ya Wafilistini iliyotawaliwa na wakubwa watano wa Wafilistini. Miji hiyo ilikuwa yenye kuzungukwa na kuta na vijiji ambavyo havikuzungushiwa kuta. Lile jiwe kubwa kwenye shamba la Yoshua wa Beti-Semesi, pahali ambapo walilipeleka Sanduku la Yawe, ni ushuhuda wa tukio hilo mpaka leo.
19Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.
Sanduku la Agano kule Kiriati-Yearimu20Kisha, wakaaji wa muji wa Beti-Semesi wakasema: “Nani anayeweza kusimama mbele ya Yawe, huyu Mungu mutakatifu? Atakwenda kwa nani kusudi aondoke kwetu?”
21Walituma wajumbe kwenda kwa wakaaji wa muji wa Kiriati-Yearimu, waseme: “Wafilistini wamelirudisha Sanduku la Yawe, mukuje mulikamate.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.