1“Halafu kwa wakati ule, Ufalme wa mbinguni utafanana na wabinti kumi waliotwaa taa zao na kwenda kumupokea bwana-arusi.
2Watano kati yao walikuwa wajinga na watano walikuwa wenye akili.
3Wale wajinga walitwaa taa zao tu, lakini hawakupeleka mafuta ya kutia ndani yao.
4Lakini wale wenye akili walitwaa machupa ya mafuta pamoja na taa zao.
5Na kwa kuona bwana-arusi alikawia kufika, wote wakasinzia na kulala usingizi.
6“Ilipokuwa katikati ya usiku, kelele likasikilika, likisema: ‘Angalia, bwana-arusi anakuja! Muondoke kwenda kumupokea!’
7Halafu wale wabinti kumi wakaamuka, wakatengeneza taa zao.
8Wale wajinga wakawaambia wenye akili: ‘Mutusaidie na mafuta kidogo, kwa sababu taa zetu zinaanza kuzimika.’
9Lakini wale wenye akili wakajibu: ‘Haiwezekani, mafuta tunayokuwa nayo hayatutoshelei. Afazali muende kwa wachuuzi na kujinunulia yenu.’
10Wale wajinga walipokwenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale wenzao watano waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika karamu ya ndoa. Kisha mulango ukafungwa.
11“Nyuma, hao wengine wakafika, na kuanza kusema: ‘Bwana, bwana, utufungulie!’
12Lakini bwana akajibu: ‘Kweli ninawaambia: mimi siwajui ninyi.’ ”
13Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.
Mufano wa watumishi watatu(Lk 19.11-27)14“Maana mambo hayo ya Ufalme wa mbinguni ni kama mutu aliyetaka kwenda safari. Yeye akawaita watumishi wake, akawagawanyia mali yake.
15Akamupatia mumoja furushi tano za zahabu, mwingine furushi mbili na mwingine furushi moja kwa kadiri ya uwezo wa kila mumoja, kisha akasafiri.
16Mara moja yule mutumishi aliyepata furushi tano, akaenda kufanya uchuuzi na mali ile, akafaidia zingine tano.
17Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili.
18Lakini yule aliyepewa furushi moja, akachimba shimo katika udongo na kuficha ile mali ya bwana wake mule.
19“Kulipopita siku nyingi, bwana wa watumishi wale akarudi, akafanya hesabu ya mali yake pamoja nao.
20Yule mutumishi aliyepewa furushi tano za zahabu, akakuja, akaleta faida ya zingine tano. Na akasema: ‘Bwana, umenipatia furushi tano za zahabu, na sasa angalia, kuna faida ya zingine tano.’
21Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’
22Halafu mutumishi aliyepewa furushi mbili akakuja, akasema: ‘Bwana, umenipatia furushi mbili; na sasa angalia, kuna faida ya zingine mbili.’
23Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mingi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako!’
24Kisha yule mutumishi aliyepewa furushi moja akakuja, akasema: ‘Bwana, nilijua kuwa wewe ni mutu mugumu anayevuna nafasi asipopanda, na kukusanya nafasi asiposambaza.
25Kwa hiyo niliogopa, nami nikaenda kuficha ile mali yako ndani ya udongo. Basi mali yako ndiyo hii, uitwae.’
26Naye bwana wake akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya na muvivu! Ulijua kama ninavuna nafasi nisipopanda, na kukusanya nafasi nisiposambaza.
27Basi, ungepaswa kuweka mali yangu ndani ya banki, kusudi siku ya kurudi kwangu, ningepata mali yangu pamoja na faida yake.
28Mumunyanganye ile furushi moja na kuitoa kwa yule anayekuwa na furushi kumi.
29Kwa maana mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine; lakini mutu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho.
30Na zaidi ya hii, mumutupe huyu mutumishi asiyekuwa na mafaa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’
Hukumu ya mataifa31“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.
32Mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atayatenga kwa makundi mawili kama vile muchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.
33Ataweka kondoo kwa upande wake wa kuume, na mbuzi kwa upande wake wa kushoto.
34Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.
35Kwa maana nilisikia njaa, mukanipa chakula; nilisikia kiu, mukanipa maji; nilikuwa mugeni, mukanikaribisha;
36nilikuwa uchi, mukanipatia nguo; nilikuwa mugonjwa, mukanisaidia; nilikuwa katika kifungo, mulikuja kuniangalia.’
37Halafu wenye haki watamujibu: ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, tukakupa chakula, au uliposikia kiu, tukakupa maji?
38Ni wakati gani tulipokuona uko mugeni, tukakukaribisha, ulipokuwa uchi, tukakupatia nguo?
39Na ni wakati gani tulipokuona uko mugonjwa au uko katika kifungo tukakuja kukuangalia?’
40Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’
41“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
42Kwa maana nilisikia njaa, nanyi hamukunipa chakula; nilisikia kiu, nanyi hamukunipa maji;
43nilikuwa mugeni, nanyi hamukunikaribisha; nilikuwa uchi, nanyi hamukunipatia nguo; nilikuwa mugonjwa na nilikuwa katika kifungo, nanyi hamukukuja kuniangalia.’
44Halafu nao watajibu: ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, au kiu, au ukikuwa mugeni, au uchi, au mugonjwa, au mufungwa, nasi hatukukusaidia?’
45Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’
46Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.