1Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahazi wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akaanza kutawala Israeli, na utawala wake uliendelea ukiwa kule Samaria kwa miaka tisa.
2Alitenda maovu mbele ya Yawe ingawa siyo kama wafalme wa Israeli waliomutangulia.
3Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.
4Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.
Kushindwa kwa Samaria5Kisha mufalme wa Asuria akashambulia inchi nzima na kuufikia muji wa Samaria na kuuzunguka kwa muda wa miaka mitatu.
6Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.
7Haya yote yalitendeka kwa sababu watu wa Israeli walimwasi Yawe, Mungu wao, ambaye aliwatoa kutoka mikono ya mufalme wa Misri, vilevile waliabudu miungu mingine,
8na kufuata njia za mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake walipokuwa wanaingia, na kufanya matendo ya wafalme wa Israeli waliyoyaingiza katika inchi.
9Watu wa Israeli walitenda kwa siri mambo yasiyokuwa mema mbele za Yawe, Mungu wao. Walijenga nafasi ya kuabudu miungu ya uongo katika kila muji, kuanzia kwenye munara wa walinzi katika mashamba mpaka katika miji yenye kuta.
10Juu ya kila kilima na chini ya kila muti wenye majani mabichi, walijenga nguzo za mawe na sanamu za miungu wa kike Ashera,
11na wakafukiza ubani kwenye mazabahu yote ya miungu ya uongo kwa kufuata desturi za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe. Walimukasirikisha Yawe na matendo yao maovu,
12na walitumikia sanamu ambazo Yawe alikuwa amewakataza, akisema: “Musifanye hivyo.”
13Yawe alituma manabii na waonaji kuionya inchi ya Israeli na ya Yuda akisema: “Mwache njia zenu mbaya mutii amri zangu na masharti yangu kufuatana na sheria nilizowapa babu zenu, na ambazo niliwapa ninyi kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14Lakini wao hawakutii; walikuwa wagumu kama babu zao ambao hawakumwamini Yawe, Mungu wao.
15Walikataa kutii masharti yake; hawakushika agano alilofanya na babu zao, walizarau maonyo yake, waliabudu sanamu zisizokuwa na maana hata wao wenyewe hawakukuwa na maana tena, walifuata desturi za mataifa yaliyowazunguka: walizarau amri za Yawe; wala hawakuzishika.
16Walivunja amri zote za Yawe, Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za miungu ya wana-ngombe wawili wa madini yenye kuyeyushwa, wakatengeneza sanamu za Ashera, wakaabudu jeshi la mbingu, na wakamutumikia Bali.
17Waliwatambikia watoto wao wa kiume na wa kike kwa miungu ya uongo; wakaomba shauri kwa watabiri na wachawi. Walijitoa kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe, wakamukasirikisha sana.
18Basi, Yawe akawakasirikia sana watu wa Israeli na kuwafukuza kabisa mbele yake; hakuacha mutu isipokuwa kabila la Yuda peke yake.
19Lakini hata watu wa Yuda hawakutii amri za Yawe, Mungu wao; lakini walifuata desturi zilizoletwa na watu wa Israeli.
20Yawe aliwakataa Waisraeli wote; akawaazibu na kuwaacha katika mikono ya waadui wakali, na kisha akawafukuza mbele yake.
21Nyuma ya Yawe kutenga Israeli kutoka ukoo wa Daudi walimuweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mufalme. Naye Yeroboamu aliwasukuma watu wa Israeli kumwacha Yawe na kutenda zambi kubwa sana.
22Waisraeli walitenda zambi zote Yeroboamu alizotenda. Hawakuziacha
23mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.
Waasuria wanafanya makao yao kule Israeli24Kisha mufalme wa Asuria akapeleka watu kutoka Babeli, Kuta, Awa, Hamati na Sefarwaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria kwa pahali pa watu wa Israeli waliopelekwa katika uhamisho. Wakaitwaa miji hiyo na kukaa mule.
25Basi ikatokea kwamba walipoanza kukaa mule, hawakumwabudu Yawe, kwa hiyo Yawe akatuma simba kati yao, nao wakawaua wamoja kati yao.
26Halafu watu wakamwambia mufalme wa Asuria, “Mataifa uliyoyakamata na kuyaweka katika miji ya Samaria hayakujua hukumu za Mungu wa inchi hiyo, kwa hiyo Mungu huyo alituma simba ambao wanawaua.”
27Halafu mufalme wa Asuria akaamuru: “Murudishe kuhani mumoja kati ya wale tuliowaleta katika uhamisho. Mumurudishe aende na kukaa kule, kusudi awafundishe watu sheria ya Mungu wa inchi hiyo.”
28Kwa hiyo, mumoja wa makuhani waliopelekwa katika uhamisho toka Samaria alikwenda na kukaa Beteli, na kule akawafundisha watu jinsi ya kumwabudu Yawe.
29Lakini mataifa yote katika miji yalimoishi yalijitengenezea miungu yao na kuiweka kwa nafasi zenye kuinuka ambako watu wa Samaria walikuwa wametengeneza.
30Watu wa Babeli walitengeneza sanamu za Sukoti-Benoti, watu wa Kuta wakatengeneza sanamu za Nergali, watu wa Hamati sanamu za Asima,
31watu wa Awa sanamu za Nibunasi na za Tartaki, na Wasefarwaimu walitoa watoto wao kuwa sadaka za kuteketezwa kwa miungu yao Adarameleki na Anameleki.
32Watu hawa vilevile walimwabudu Yawe. Walichagua kutoka kati yao watu wa kila aina na kuwafanya makuhani kutumika katika nafasi zenye kuinuka juu na kutoa sadaka kule kwa ajili yao.
33Hivi wakamwabudu Yawe, lakini wakati uleule wakiwaabudu vilevile miungu yao waliyoleta kutoka inchi zao.
34Hata sasa wanatenda kama vile walivyofanya zamani. Hawamwabudu Yawe, wala hawafuati masharti, maagizo, sheria au amri ambazo yeye Yawe aliwaamuru wana wa Yakobo; ambaye alimupa jina la Israeli.
35Yawe alikuwa amefanya agano nao na kuwaamuru: “Musiabudu miungu mingine; musiiname mbele yake, musiitumikie wala musiitambikie.
36Mutaniabudu mimi Yawe, ambaye niliwatoa kule Misri kwa uwezo na nguvu nyingi. Mutainama mbele yangu mimi na kunitolea sadaka.
37Wakati wote mutatii masharti, maagizo, sheria na amri ambazo niliandika kwa ajili yenu, siku zote mutakuwa waangalifu kwa kuzitenda. Musiiabudu miungu mingine,
38wala musisahau agano nililofanya nanyi, musiiabudu miungu mingine, lakini
39mutaniabudu mimi Yawe, Mungu wenu, nami nitawaokoa kutoka katika mikono ya waadui zenu.”
40Lakini watu hao hawakusikiliza, wao waliendelea kutenda kama vile walivyofanya zamani.
41Basi mataifa haya yalimwabudu Yawe, lakini vilevile walitumikia sanamu zao za madini yenye kuyeyushwa; na mpaka sasa hivi, wazao wao wanaendelea kutenda hivyo kama vile babu zao walivyotenda.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.