1“Mumupende Yawe, Mungu wenu, na kushika siku zote masharti yake, maagizo yake na amri zake.
2Mufikiri kwa uangalifu, kwa sababu ya watoto wenu ambao hawakujua wala hawakuona azabu ya Yawe, uwezo wake na nguvu zake,
3vitambulisho vyake na maajabu yake aliyotenda kule Misri kwa mufalme wa Misri na inchi yake yote,
4aliyotendea jeshi la Misri, farasi wao na magari yao ya vita, jinsi alivyozamisha jeshi hilo katika bahari Nyekundu, na jinsi Yawe alivyoliangamiza hata hivi leo.
5Mukumbuke jinsi Yawe aliyowafanyia ninyi katika jangwa mbele hamujafika hapa,
6na mambo aliyowatendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu, mwana wa Rubeni. Mukumbuke jinsi mbele ya watu wote wa Israeli udongo ulivyofunguka na kuwameza pamoja na jamaa zao, mahema yao, nyama na watumishi wao wote.
7Maana macho yenu yameona matendo yote haya makubwa ambayo Yawe alifanya.
Neema za inchi ya ahadi8“Mutii amri zote ninazowaamuru siku hii ya leo, kusudi mupate kuingia na kurizi inchi munayoiendea,
9mupate kuishi kwa muda murefu katika inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ambayo Yawe aliahidi kuwapa babu zenu na wazao wao.
10Inchi munayokwenda kurizi si kama inchi ya Misri mulikotoka, ambako mulipanda ngano nanyi mulipaswa kuleta maji kutoka kwenye mito kwa kuimwangilia kama vile mulivyofanya kwa mashamba ya mboga.
11Lakini inchi munayokwenda kurizi ni inchi ya milima na mabonde, inchi ambayo inapata maji ya mvua kutoka mbinguni,
12inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anatunza. Siku zote anaiangalia tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka.
13“Basi, mukitii amri zangu ninazowapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kumutumikia kwa moyo wenu wote na kwa roho yenu yote,
14yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.
15Ataotesha majani katika mashamba kwa ajili ya ngombe wenu, nanyi mutakula na kushiba.
16Mufanye angalisho kusudi mioyo yenu isidanganywe, mukigeuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu,
17nayo hasira ya Yawe iwake juu yenu, naye afunge mbingu hata kusikuwe mvua, na inchi iache kutoa mazao yake, halafu muangamie upesi kutoka katika inchi nzuri ambayo Yawe anawapa.
18“Muweke maneno yangu haya ndani ya mioyo yenu na roho zenu. Muyafungie katika mikono yenu kama vile kitambulisho na kuyavaa katika paji la uso.
19Muwafundishe watoto wenu maneno haya mukiyazungumuzia munapoikaa katika nyumba zenu, munapotembea, munapolala na munapoamuka.
20Muyaandike kwenye miimo ya milango yenu na milango ya miji yenu,
21kusudi ninyi na watoto wenu mupate kuishi maisha marefu katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, aliapa kuwapa babu zenu, siku zote mbingu zitakapodumu juu ya dunia.
22“Kama mukishika amri zote ambazo nimewapa, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake zote na kuambatana naye,
23basi Yawe atafukuza mataifa yote hayo mbele yenu, nanyi mutarizi inchi inayokuwa mali ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi.
24Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.
25Hakuna mutu yeyote atakayeweza kuwashambulia. Popote mutakapokwenda katika inchi hiyo, Yawe, Mungu wenu, atawatia watu hofu wawaogope, kama vile alivyowaahidi.
26“Leo hii ninawawekea mbele yenu baraka na laana:
27baraka, kama mutatii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa hivi leo;
28na laana, kama hamutatii amri za Yawe, Mungu wenu, na kuacha njia ninayowaamuru, mukiabudu miungu mingine ambayo hata hamujajua bado.
29Yawe atakapowafikisha kwenye inchi munayokwenda kurizi, mutatangaza baraka kutoka kwenye mulima Gerizimu, na laana kutoka kwenye mulima Ebali.
30(Milima hii iko ngambo ya muto Yordani, upande wa magaribi wa barabara kuelekea upande jua linakotokea, katika inchi ya Wakanana wanaoishi Araba kuelekea Gilgali.)
31Maana mutavuka muto Yordani muingie kwa kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa. Basi mutakapoirizi na kukaa humo,
32muangalie kwamba munatimiza masharti yote na maagizo ambayo ninawapa leo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.