1Kisha Yawe akamwambia Yoshua, Ang. Hes 35.6-32; Kumb 4.41-43; 19.1-13
2awaambie Waisraeli hivi: “Mujichagulie miji ambamo mutu anaweza kukimbilia usalama ambayo nilimwambia Musa akuelezee.
3Mutu yeyote akimwua mutu bila kukusudia anaweza kukimbilia katika muji mumoja na hivyo anaweza kuepuka yule mutu anayekuwa na ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu.
4Mwuaji atakimbilia katika muji mumoja wa miji ile na kusimama kwenye mulango wa muji na kuwaelezea wazee wa muji ule maneno yake. Wazee watamupokea ndani na kumupa pahali pa kuishi pamoja nao.
5Kama yule mutu mwenye kuwa na ruhusa ya kulipiza kisasi akimufuatilia mpaka katika muji ule, wazee wa muji ule hawaruhusiwi kumutoa mwuaji yule kwa yule mwenye kutaka kulipiza kisasi maana alimwua mwenzake kwa bahati mbaya tu kwa vile hakukukuwa uadui kati yao zamani.
6Mwuaji ataendelea kuishi mule mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wote wa Waisraeli na vilevile mpaka pale yule Kuhani Mukubwa ambaye alikuwa na madaraka wakati ule atakapokufa. Nyuma ya pale mutu huyo ataweza kurudi katika nyumba yake katika muji ule pahali alipotoka wakati alipotoroka.”
7Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.
8Na ngambo ya muto Yordani, upande wa mashariki wa muji wa Yeriko, walichagua muji wa Bezeri unaokuwa kwenye jangwa katika mabonde ya eneo la kabila la Rubeni. Vilevile wakachagua Ramoti, kule Gileadi ambao ni muji wa kabila la Gadi na Golani kule Basani katika eneo la kabila la Manase.
9Hii ndiyo miji iliyotengwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na wageni walioishi kati yao, kusudi mutu yeyote atakayemwua mwenzake bila kukusudia akimbilie kule asipate kuuawa na mwenye ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu, mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wa watu wote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.