1Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, akatawala kutoka Yerusalema kwa muda wa miaka makumi tano na mitano.
2Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kuiga mienendo miovu ya mataifa ambayo Yawe aliyafukuza wakati watu wake wa Israeli walipokuwa wanaingia. Ang. Yer 15.4
3Kwa maana alijenga tena pahali pa kuabudia miungu mingine palipokuwa pamebomolewa na baba yake Hezekia; akajenga mazabahu za kuabudia Mabali, na kutengeneza sanamu za Ashera. Vilevile, aliabudu jeshi la mbinguni na kulitumikia.
4Alijenga tena mazabahu katika nyumba ya Yawe pahali ambapo Yawe alikuwa amesema: “Jina langu litaabudiwa milele katika Yerusalema.” Ang. 2 Sik 6.6
5Alijenga mazabahu za kuabudia jeshi la mbinguni kwenye viwanja vya nyumba ya Yawe.
6Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.
7Nayo sanamu aliyotengeneza, akaiweka katika nyumba ya Mungu ambayo aliizungumuzia, mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema kati ya makabila kumi na mawili ya Israeli, ndipo pahali nitakapoabudiwa milele. Ang. 1 Fal 9.3-5; 2 Sik 7.12-18
8Na ikiwa watu wa Israeli watajali kutenda yote niliyowaamuru, Sheria yote, masharti, na maagizo yaliyotolewa kwa mukono wa Musa, basi sitawaacha hata kidogo wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”
9Lakini Manase aliwapotosha watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema, wakatenda maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yawe aliyaangamiza mbele ya watu wa Israeli.
Manase anatubu10Yawe akamwonya Manase na watu wake, lakini hawakumusikia.
11Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.
12Wakati alipokuwa katika taabu, akamwomba Yawe, Mungu wake rehema. Akajinyenyekeza sana mbele ya Mungu wa babu zake.
13Alimusihi, naye Mungu akapokea maombi yake na kusihi kwake, akamurudisha Yerusalema katika ufalme wake. Halafu Manase akatambua kwamba Yawe ndiye Mungu.
14Nyuma ya hayo, Manase akajenga ukuta mwingine upande wa inje wa muji wa Daudi, upande wa magaribi wa Gihoni, katika bonde, akauendelesha mpaka kwenye Mulango wa Samaki, akauzungusha Ofeli; akauinua juu sana. Pamoja na hayo, akaweka majemadari wa majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta.
15Akatoa katika nyumba ya Yawe miungu yote ya kigeni na sanamu pamoja na mazabahu zote alizokuwa amejenga kwenye mulima wa nyumba ya Yawe na katika Yerusalema; akavitupa inje ya muji.
16Akarudisha mazabahu ya kumwabudia Yawe, na juu yake akatoa sadaka za amani na za shukrani, akawaamuru watu wa inchi ya Yuda wamwabudu Yawe, Mungu wa Israeli.
17Hata hivyo watu wakaendelea kutoa sadaka kwenye nafasi ya kufanyia ibada, lakini kwa Yawe, Mungu wao tu.
Mwisho wa utawala wa Manase(2 Fal 21.17-18)18Matendo mengine ya Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno ya waonaji waliozungumuza naye katika jina la Yawe, Mungu wa Israeli, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Wafalme wa Israeli.
19Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.
20Manase alikufa na kuzikwa katika nyumba yake ya kifalme, naye Amoni, mwana wake, akatawala pahali pake.
Mufalme Amoni wa Yuda(2 Fal 21.19-26)21Amoni alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na miwili alipoanza kutawala inchi ya Yuda, alitawala miaka miwili akiwa kule Yerusalema.
22Alitenda maovu mbele ya Yawe, kama vile baba yake Manase alivyofanya. Vilevile alitoa sadaka na kutumikia sanamu ambazo baba yake Manase alichonga.
23Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.
24Kisha watumishi wake walimufanyia shauri baya na kumwua katika nyumba yake ya kifalme.
25Lakini watu wa inchi ya Yuda wakawaua wale wote waliomufanyia Amoni shauri baya, kisha wakamufanya Yosia, mwana wake kuwa mufalme pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.