1Sasa juu ya muchango unaofanyika kwa ajili ya watu watakatifu wa Mungu wanaokuwa Yerusalema; ninyi vilevile mufanye sawa vile nilivyoagiza makanisa ya Galatia.
2Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.
3Nami nitakapofika, nitatuma watu mutakaochagua, pamoja na barua kwa kupeleka zawadi yenu Yerusalema.
4Ikiwa ni lazima mimi niende vilevile, basi nitasafiri pamoja nao.
Mipango ya Paulo5Nitakuja kwenu kisha kupitia Makedonia kufuatana na mupango wangu wa kupitia kule.
6Labda nitabakia pamoja nanyi muda kidogo, au tena wakati wote wa mvua kali; kusudi muweze kunisaidia kuendelea pahali popote nitakapokwenda.
7Kwa maana sitaki kuonana nanyi kwa kupita tu. Ninatumaini kukaa pamoja nanyi siku chache Bwana akitaka.
8Lakini, ninataka kubakia hapa Efeso, mpaka siku ya Pentekoste.
9Kwa maana nimepata hapa wakati muzuri wa kufanya kazi kubwa ijapokuwa wapinzani ni wengi.
10Kama Timoteo akifika, mujikaze kumupokea vizuri kati yenu kwa sababu yeye anafanya kazi ya Bwana kama mimi mwenyewe.
11Basi hata mutu mumoja asimuzarau. Lakini mumusaidie aendelee na safari yake katika amani; kusudi apate kurudia kwangu, maana ninamungojea yeye pamoja na wandugu waamini.
12Kwa ngambo ya ndugu yetu Apolo, nimemusihi sana akuje kwenu pamoja na wandugu wengine, lakini hakutaka kabisa kwenda sasa; atakwenda kwa wakati utakaomupendeza.
Maneno ya mwisho na salamu13Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.
14Mutende mambo yenu yote katika upendo.
15Ninyi munajua Stefana na jamaa yake; munafahamu kwamba walikuwa watu wa kwanza walioamini katika inchi ya Akaya, nao wamejitoa kwa kutumikia watu wa Mungu. Hivi ninawasihi sana wandugu zangu,
16mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.
17Nami ninafurahi kwa kufika kwa Stefana, Fortunato na Akaiko; wamekuwa kwa pahali penu,
18nao wamenifariji kama vile walivyowafariji ninyi wenyewe. Inafaa kuwakumbuka watu kama hawa.
19Makanisa ya jimbo la Azia yanawasalimia. Akila na Prisila pamoja na kanisa linalokusanyika ndani ya nyumba yao wanawasalimia sana katika Bwana.
20Wandugu wote wanaokuwa hapa wanawasalimia. Na ninyi vilevile musalimiane kwa upendo wa kikristo.
21Hii ni salamu ninayoiandika kwa mukono wangu mimi Paulo mwenyewe.
22Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe!
Bwana wetu, kuja!
23Neema ya Bwana Yesu ikuwe pamoja nanyi.
24Ninawapenda ninyi wote katika kuungana na Yesu Kristo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.