Wimbo wa Solomono 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Ninaingia katika bustani yangu,

dada yangu, muchumba wangu.

Ninakusanya manemane na majani yenye harufu,

ninakula sega langu la asali,

ninakunywa divai yangu na maziwa yangu.

Masemi ya muke

Mukule, enyi warafiki, mukunywe;

mukunywe sana, wapendwa wangu.

Shairi la ineMasemi ya muke

2Nililala usingizi, lakini moyo wangu ulikesha.

Nikasikia mupenzi wangu akipiga hodi.

Masemi ya mume

Unifungulie dada, ee mupenzi wangu, muchumba wangu,

njiwa yangu, usiyekuwa na kilema chochote.

Kichwa changu kimelowana na umande

na nywele zangu na manyunyu ya usiku.

Masemi ya muke

3Nimekwisha kuvua nguo zangu,

nitazivaa namna gani tena?

Nimekwisha kunawa miguu yangu,

niichafue namna gani tena?

4Halafu mupenzi wangu akaugusa mulango,

moyo wangu ukajaa furaha.

5Nikasimama kwa kumufungulia mupenzi wangu.

Mikono yangu ikajaa manemane,

na vidole vyangu vikadondosha manemane,

nikashika kifungio kwa kufungua mulango.

6Nikamufungulia mupenzi wangu mulango,

lakini kumbe, alikuwa amekwisha kutoweka.

Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumuza!

Nikamutafuta, lakini sikumupata;

nikamwita, lakini hakuniitikia.

7Walinzi wa muji walinikuta,

walipokuwa wakizunguka katika muji.

Wakanipiga na kuniumiza;

nao walinzi wa mulango wakaninyanganya ushungi wangu.

8Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,

mukimwona mupenzi wangu,

mumwelezee kwamba ninaugua kwa ajili ya mapenzi!

Wabinti

9Ewe unayependeza kuliko wabinti wote,

huyo mupenzi wako ana nini cha zaidi ya mupenzi mwingine,

hata utusihi kwa moyo mpaka pale?

Masemi ya muke

10Mupenzi wangu ni muzuri na ni mwekundu,

anatambulikana kati ya wanaume elfu kumi.

11Kichwa chake ni kizuri kama zahabu safi,

nywele zake ni zenye kulembelea,

nyeusi sana kama kibombobombo.

12Macho yake ni kama ya njiwa kandokando ya kijito,

ni kama njiwa waliooga maziwa pembeni ya kijito.

13Mashavu yake ni kama bustani inayojaa marasi,

yenye harufu nzuri.

Midomo yake ni kama yungiyungi,

inatonatona manemane kwa wingi.

14Mikono yake ni kama pete za zahabu,

amevaa mawe ya bei kali.

Kiwiliwili chake ni kama pembe za tembo

zilizopambwa kwa mawe ya yakuti ya rangi ya samawi.

15Miguu yake ni kama nguzo za mawe meusi,

zilizosimikwa katika misingi ya zahabu.

Umbo lake ni kama mulima Lebanoni,

ni bora kama miti ya mierezi.

16Kinywa chake kinajaa maneno matamu.

Yeye wote anapendeza.

Basi, hivi ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa,

ndivyo rafiki yangu anavyokuwa,

enyi wabinti wa Yerusalema.

Wabinti
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help