Isaya 10 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Ole kwao wanaotunga sheria za uovu,

watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.

2Wanakataa kusambisha wazaifu,

wananyanganya watu wangu wamasikini haki yao.

Wanateka wajane;

wananyanganya wayatima mali yao.

3Mutafanya nini siku ya azabu,

siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali?

Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada?

Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?

4Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa

na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita.

Hata hivyo, hasira yake haijatulia,

angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.

Maonyo kwa mufalme wa Asuria

5Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu,

yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!

6Nilimutuma kuliazibu taifa ovu,

nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia,

kuwanyanganya na kuteka vitu vyao,

na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.

7Lakini Asuria hakuwazia hivyo,

yeye alikuwa na nia ingine;

alikusudia kuharibu kabisa,

kuangamiza mataifa mengi sana.

8Maana alisema:

Si kweli majemadari wangu ni wafalme?

9Si kweli kwamba muji wa Kalno niliutendea kama vile wa Karkemisi,

muji wa Hamati kama muji wa Arpadi,

Samaria kama Damasiki?

10Nimepata kuunyoosha mukono wangu

juu ya falme zenye sanamu za miungu

kubwa kuliko sanamu za Yerusalema na Samaria.

11Basi nitashindwa kuutendea Yerusalema na sanamu zake,

kama nilivyoutendea Samaria na sanamu zake?

12Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.

13Maana mufalme wa Asuria alisema:

Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo,

na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu!

Nimeondoa mipaka kati ya mataifa,

nikanyanganya akiba zao;

kama ngombe dume nimewaporomosha walioikaa juu ya viti vya kifalme.

14Kama mutu anayenyoosha mukono kwenye chicha,

ndivyo nilivyokamata mali ya mataifa;

kama mutu anayeokota mayai yaliyoachwa ndani ya chicha,

ndivyo nilivyoyaokota katika dunia yote.

Watu wote walikuwa sawa ndege ambaye hapigi mabawa

au kufungua midomo kwa kupiga kelele.

Lakini Yawe anasema hivi:

15Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia?

Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao?

Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika,

au gongo kumwinua mwenye kuitumia!

16Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi,

atawaletea waaskari wao wanene ugonjwa wa kuwakondesha,

na utukufu wao utateketezwa kama kwa moto.

17Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto.

Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto

ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu,

miiba yake na michongoma zake pamoja.

18Pori yake yenye utukufu na mashamba yake mazuri,

Yawe atayaangamiza yote;

itakuwa kama mutu aliyemalizika na ugonjwa.

19Miti itakayobaki katika pori yake itakuwa michache sana

hata mutoto mudogo ataweza kuihesabu.

Wachache watarudi

20Siku ile wazao wa Yakobo watakaobaki, ni kusema Waisraeli watakaopona hawatalitegemea tena taifa lililowaazibu, lakini watamutegemea kabisa Yawe, Mutakatifu wa Israeli.

21Wazao wa Yakobo wachache watakaobaki watamurudilia Mungu Mukubwa.

22Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu. Ang. Rom 9.27

23Kweli! Bwana, Yawe wa majeshi, atakamilisha kabisa katika inchi yote jambo aliloamua kutenda.

Yawe ataiazibu inchi ya Asuria

24Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.

25Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.

26Yawe wa majeshi atainua fimbo yake kama vile alivyowapiga Wamidiani kwenye jiwe la Orebu. Atanyoosha fimbo yake juu ya bahari kama vile alivyowafanyia Wamisri.

27Wakati huo, muzigo waliowabebesha atauondoa na nira waliyowatia kwenye shingo lenu itavunjwa.

Adui anakaribia

Adui amepanda kutoka Rimoni,

28amefika katika muji wa Ayati.

Amepitia kule Migoroni,

mizigo yake ameiacha katika muji wa Mikimasi.

29Amekwisha pita kwenye kivuko.

Usiku huu analala Geba.

Watu wa Rama wanatetemeka kwa hofu,

wakaaji wa Gibea, muji wa Sauli, wamekimbia.

30Enyi watu wa Galimu, mupige kelele!

Enyi watu wa Laisi, mutege sikio!

Enyi wenyeji wa Anatoti, mujibu!

31Watu wa Madimena wamekimbia,

wakaaji wa Gebimu wanatafuta makimbilio.

32Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba,

anainua mukono wake kwa mulima Sayuni,

kilima cha Yerusalema.

33Bwana, Yawe wa majeshi

atakata matawi kwa ukali,

miti mirefu itaangushwa chini,

wanaokuwa juu watashushwa.

34Atakata vichaka vya pori kwa shoka;

Lebanoni na mierezi yake yenye utukufu itaanguka.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help