Waamuzi 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ugomvi kati ya Yefuta na kabila la Efuraimu

1Watu wa kabila la Efuraimu wakakusanyika, wakavuka muto Yordani wakafika kule Safoni. Kisha wakamwambia Yefuta: “Kwa nini haukutuita tuende pamoja nawe kupigana na Waamoni? Sasa tutaichoma nyumba yako nawe mwenyewe ndani yake.”

2Yefuta akawaambia: “Mimi pamoja na watu wangu tulikuwa na uadui mukubwa na Waamoni. Niliwaomba munisaidie lakini hamukukuja kuniokoa.

3Nilipoona kwamba hamukukuja kuniokoa, nikahatarisha maisha yangu, nikavuka kwenda kupigana na Waamoni, naye Yawe akawatia katika mikono yangu. Kwa nini sasa munakuja kupigana na mimi?”

4Basi, Yefuta akakusanya watu wote wa Gileadi, akapigana na watu wa Efuraimu. Watu wa Gileadi wakawashinda watu wa Efuraimu. Hawa Waefuraimu ndio hao waliokuwa wamesema: “Ninyi watu wa Gileadi ni wakimbizi wa kabila la Efuraimu muliotoka katika kabila la Efuraimu mukaenda kwa kabila la Manase.”

5Kisha watu wakavishika vivuko vya muto Yordani kwa kuiziba njia ya watu wa Efuraimu. Kila mara mukimbizi alipotokea akiomba kupita kule, watu wa Gileadi walimwuliza: “Wewe ni Mwefuraimu?” Na kama akijibu “Hapana”,

6walimwambia: “Basi useme neno ‘Shiboleti’ ”. Lakini yeye akisema “Siboleti” kwa sababu hakuweza kulitamka sawasawa, walimukamata na kumwua kule kwenye vivuko vya muto Yordani. Watu elfu makumi ine na mbili wa Efuraimu wakapoteza maisha yao wakati ule.

7Yefuta alikuwa mwamuzi katika Israeli kwa miaka sita. Kisha akakufa, akazikwa kule Gileadi katika muji wake.

Ibusani, Eloni, na Abudoni

8Nyuma ya Yefuta, Ibusani wa muji wa Betelehemu akakuwa mwamuzi wa Israeli.

9Yeye alikuwa na wana makumi tatu na wabinti makumi tatu. Nao wabinti zake aliwaoesha inje ya ukoo wake, na wana aliwaoea wabinti makumi tatu kutoka inje ya ukoo wake. Ibusani alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka saba.

10Akakufa, akazikwa katika muji wa Betelehemu.

11Nyuma ya Ibusani, Eloni wa kabila la Zebuluni, akakuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka kumi.

12Naye akakufa, akazikwa katika muji wa Ayaloni katika inchi ya kabila la Zebuluni.

13Nyuma ya Eloni, Abudoni mwana wa Hileli wa muji wa Piratoni akakuwa mwamuzi wa Israeli.

14Yeye alikuwa na watoto wanaume makumi ine na wajukuu makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi saba. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka minane.

15Kisha Abudoni akakufa, akazikwa katika muji wa Piratoni katika inchi ya kabila la Efuraimu kwenye eneo la milima ya Waamaleki.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help