1Watu wa Israeli walipotoka Misri,
wazao wa Yakobo walipotoka katika inchi ya kigeni,
2Yuda ikakuwa makao ya Mungu,
Israeli ikakuwa urizi wake.
3Bahari iliona hayo ikakimbia;
muto Yordani ukaacha kutiririka!
4Milima ilirukaruka kama kondoo dume;
vilima vikaruka kama wana-kondoo!
5Ee bahari, nini iliyokufikia hata ukakimbia?
Nawe Yordani, kwa nini uliacha kutiririka?
6Enyi milima, mbona muliruka kama kondoo dume?
Nanyi vilima, namna gani mumeruka kama mwana-kondoo?
7Utetemeke, ee dunia, mbele ya Yawe;
utetemeke mbele ya Mungu wa Yakobo,
8anayegeuza jiwe kubwa kuwa ziwa,
nalo jiwe gumu kuwa chemichemi za maji!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.