1Yetro, kuhani wa Midiani, baba mukwe wa Musa, alisikia juu ya mambo yote ambayo Yawe alimutendea Musa na Waisraeli alipowatoa katika inchi ya Misri.
2Kwa hiyo Yetro, akiwa na Sipora muke wa Musa ambaye Musa alikuwa amemurudisha kwa baba yake, alimwendea Musa, katika inchi ya kigeni.” , kwa vile Musa alisema: “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na mufalme wa Misri.”
5Yetro, baba mukwe wa Musa, alikuja pamoja na binti yake, ni kusema muke wa Musa, pamoja na watoto. Akamukuta Musa katika jangwa alikokuwa amepiga kambi kwenye mulima wa Mungu.
6Musa alipoambiwa kwamba baba mukwe wake pamoja na muke wake na wana wake wawili wanakuja,
7akatoka kwenda kumupokea baba mukwe wake, akiinama mbele yake na kumubusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia ndani ya hema.
8Musa akamwelezea baba mukwe wake mambo yote Yawe aliyomutendea mufalme wa Misri na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli. Akamwambia vilevile juu ya shida zote zilizowapata katika safari na jinsi Yawe alivyowaokoa.
9Yetro akafurahishwa na yote Yawe aliyotenda kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwaokoa toka katika mikono ya Wamisri.
10Yetro akasema: “Atukuzwe Yawe ambaye amewaokoa toka katika mikono ya Wamisri na kutoka katika mukono wa mufalme wa Misri.
11Sasa ninajua kwamba Yawe ni mukubwa kuliko miungu yote, maana amewakomboa watu hawa toka katika mikono ya Wamisri ambao waliwatendea ubaya.”
12Halafu Yetro, baba mukwe wa Musa, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Naye Haruni akakuja pamoja na wazee wa Israeli kwa kula chakula pamoja na Yetro, mbele ya Yawe.
Kuchaguliwa kwa waamuzi(Kumb 1.9-18)13Kesho yake, Musa akaikaa kwa kuamua matatizo ya Waisraeli, nao wakasimama wakiwa wamemuzunguka, tangu asubui mpaka magaribi.
14Yetro, baba mukwe wa Musa, alipoona mambo yote ambayo Musa aliwafanyia Waisraeli, akamwuliza: “Kwa nini unawafanyia watu mambo haya? Mbona unaikaa peke yako wakati watu wamekuzunguka tangu asubui mpaka magaribi?”
15Musa akamujibu baba mukwe wake: “Kwa sababu watu wanakuja kwangu kuuliza mapenzi ya Mungu.
16Wakiwa na ugomvi wowote wao wanakuja kwangu nami ninaamua kati ya mutu na mwenzake na kuwafundisha masharti ya Mungu na maamuzi yake.”
17Basi, Yetro akamwambia Musa: “Unavyofanya si vizuri!
18Utajichokesha mwenyewe na hawa watu, maana hii ni kazi ngumu usiyoweza kuifanya peke yako.
19Sikiliza shauri langu kwako na Mungu akuwe pamoja nawe. Wewe utawasimamia watu mbele ya Mungu na kumuletea Mungu matatizo yao.
20Vilevile utawafundisha masharti na sheria ya Mungu na kuwaonyesha jinsi inavyowapasa kuishi na kufanya.
21Lakini juu ya mambo mengine, chagua kati ya watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomwogopa Mungu, waaminifu na wanaochukia kituliro. Uwape hao mamlaka, wakuwe na kazi ya kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, makumi tano na kumikumi.
22Hao ndio watakaokuwa na vikao kila siku kutatua matatizo ya watu. Matatizo magumu watakuletea wewe, lakini yale madogomadogo watayaamua wenyewe. Kwa njia hiyo utaweza kufanya kazi yako kuwa nyepesi kwa vile watashirikiana nawe katika kazi hiyo.
23Ukifanya hivyo na kama ndivyo Mungu anavyotaka, utaweza kuvumilia na watu hawa wote wataweza kurudi kwao kwa amani.”
24Musa akasikiliza shauri lile la baba mukwe wake na kufanya kama vile alivyoshauriwa.
25Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.
26Nao wakakuwa wanaamua matatizo ya watu kila wakati. Matatizo magumu walimuletea Musa, lakini yale madogomadogo waliyatatua wao wenyewe.
27Kisha kufanya hivyo, Musa na baba mukwe wake wakaagana, naye Yetro akarudi katika inchi yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.