Mezali 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.

2Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.

3Mutu hawezi kudumu katika kutenda maovu, lakini hakuna kitu kinachoweza kumwangusha mutu wa haki.

4Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.

5Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.

6Maneno ya waovu shabaha yake ni kuua, lakini kinywa cha mutu wa usawa kinaokoa.

7Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.

8Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.

9Afazali mutu wa chini anayejitegemea kuliko yule anayejitakia makubwa na kukosa chakula.

10Mutu mwenye haki anajali nyama wake, lakini huruma za waovu ni kutesa tu.

11Mulimaji mwenye bidii ana chakula tele, lakini anayefuata mambo yasiyofaa hana akili.

12Matumaini ya waovu yanaporomoka na kuharibika, lakini mutu mwenye haki anasimama imara.

13Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.

14Mutu anafanikiwa kutokana na maneno yake kama vile anavyopata matokeo ya kazi za mikono yake.

15Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.

16Ujinga wa mupumbafu unajulikana mara moja, lakini mwerevu anazarau matusi.

17Musema kweli anatoa ushuhuda wa kweli, lakini mushuhuda wa uongo anasema udanganyifu.

18Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.

19Ukweli unadumu milele, lakini uongo ni wa muda kidogo tu.

20Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu ndani ya moyo, lakini wanaokusudia mema wana furaha.

21Wenye haki hawapatwi na jambo lolote baya, lakini waovu wanapata hasara nyingi.

22Kinywa kinachosema uongo ni chukizo kwa Yawe, lakini watu waaminifu ni furaha yake.

23Mutu mwerevu anaficha maarifa yake, lakini wapumbafu wanatangaza upumbafu wao.

24Kuwa na bidii kutamupa mutu cheo, lakini uvivu utamufanya mutumwa.

25Wasiwasi ndani ya moyo inamukosesha mutu raha, lakini neno zuri linamuchangamusha.

26Mutu wa haki anaepuka uovu, lakini njia ya waovu inawapotosha wenyewe.

27Mwindaji muvivu hatapata anachowinda, lakini mwenye bidii atafanikiwa.

28Haki ni njia ya uzima, lakini uovu unaongoza katika kifo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help