1Zaburi ya Daudi.
Ninakulilia,
ee Yawe!
Ewe kikingio changu, usikuwe kama kiziwi kwangu.
Usikuwe kama haunisikilizi,
nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.
2Sikiliza sauti ya ombi langu,
ninapokulilia unisaidie,
ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.
3Usiniazibu pamoja na watu wabaya,
wale watenda maovu wanaosema vizuri na wenzao,
kumbe wanajaa ubaya ndani ya moyo.
4Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao,
kufuatana na maovu waliyotenda.
Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao wenyewe;
uwatendee yale wanayostahili.
5Hawashuguliki na matendo ya Yawe;
hawatambui mambo aliyofanya.
Kwa sababu hiyo atawabomoa,
wala hatawajenga tena upya.
6Atukuzwe Yawe,
maana amesikiliza ombi langu.
7Yawe ndiye nguvu na ngao yangu;
tegemeo la moyo wangu ni kwake.
Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote;
kwa wimbo wangu ninamushukuru.
8Yawe ni nguvu ya watu wake;
yeye ni kimbilio la mufalme aliyemuchagua.
9Ee Mungu, uwaokoe watu wako;
uwabariki watu hao wanaokuwa mali yako.
Ukuwe muchungaji wao na kuwalinda milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.