Ufunuo 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Miaka elfu moja

1Kisha nikaona malaika mumoja akishuka toka mbinguni. Yeye alikuwa akishika katika mukono wake ufunguo wa shimo ndefu la kuzimu na munyororo mukubwa.

2Akamukamata yule nyoka mukubwa, ndiye yule nyoka wa zamani, anayeitwa “Mwovu” au “Shetani” na kumufunga kwa muda wa miaka elfu moja.

3Malaika yule akamutupa ndani ya shimo ndefu la kuzimu. Akalifunga na kutia kitambulisho cha muhuri juu yake kwamba lisifunguliwe kusudi nyoka yule asiyadanganye tena mataifa mpaka ile miaka elfu moja ipate kutimia. Kisha miaka hiyo, anapaswa kufunguliwa tena kwa muda mufupi.

4Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.

5(Wafu wengine waliobaki, hawakufufuka mpaka ile miaka elfu moja ipate kutimia.) Huu ndio ufufuko wa kwanza.

6Heri na baraka sana kwa wale watakaokuwa katika ufufuko wa kwanza! Kifo cha pili hakina uwezo juu yao, nao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka elfu moja.

7Wakati ile miaka elfu moja itakapotimia, Shetani atafunguliwa toka katika kifungo chake,

8naye atakwenda kuwadanganya watu wa mataifa wanaokuwa katika pande zote za dunia, ndio wanaoitwa Gogi na Magogi. Shetani atawakusanya kwa kupigana vita, nao watakuwa wengi kama vile muchanga wa bahari.

9Walitawanyika katika dunia yote, na kuzunguka kambi ya watu wa Mungu na muji wake alioupenda. Lakini moto ukashuka toka mbinguni, ukawateketeza.

10Kisha yule Mwovu aliyewadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na lenye mawe ya kiberiti yanayowaka moto, pahali yule nyama wa ajabu na yule nabii wa uongo wanapokuwa. Nao watateswa muchana na usiku, milele na milele.

Hukumu ya mwisho

11Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.

12Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.

13Bahari ikawarudisha wafu waliozama ndani yake. Kifo na kuzimu zikarudisha wafu waliokuwa ndani yao. Na kila mumoja akahukumiwa kufuatana na matendo yake.

14Kisha kifo na kuzimu vikatupwa katika ziwa la moto. Ziwa lile la moto ndicho kifo cha pili.

15Na mutu yeyote ambaye jina lake lililokosa kuandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help