1Mufalme Yabini wa muji wa Hazori alipopata habari hizo, alipeleka ujumbe kwa mufalme Yobabu wa Madoni, kwa mufalme wa Simuroni na mufalme wa Akisafu,
2na kwa wafalme waliokuwa katika milima ya upande wa kaskazini, waliokuwa Araba ambayo ilikuwa upande wa kusini wa Kineroti, kwenye mabonde na waliokuwa Nafoti-Dori katika upande wa magaribi.
3Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.
4Basi, wakatoka wote na makundi yao makubwa ya waaskari. Nao walikuwa wengi kama muchanga wa bahari pamoja na magari mengi na farasi wengi sana.
5Wafalme hawa wote wakaungana na kupiga kambi yao katika chemichemi ya Meromu kusudi wapigane na Waisraeli.
6Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”
7Basi, kwa rafla kwenye chemichemi ya Meromu, Yoshua pamoja na waaskari wake wote akawatokea na kuwashambulia.
8Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.
9Yoshua akakatakata mishipa ya miguu ya farasi wao wote na kuyateketeza magari yao kwa moto, kama Yawe alivyomwagiza.
10Yoshua alipokuwa anarudi, akauteka muji wa Hazori. Akamwua mufalme wake maana ndiye aliyekuwa kiongozi wa falme hizo zote.
11Kisha akauteketeza muji wa Hazori kwa moto na kuwaua wakaaji wake wote, hakumwacha hata mutu mumoja.
12Vilevile aliiteketeza miji ile mingine yote kwa moto na kuwaua wafalme wao wote kama vile Musa, mutumishi wa Yawe, alivyomwamuru.
13Lakini Waisraeli hawakuiteketeza miji iliyokuwa kwenye vilima, isipokuwa tu muji wa Hazori ambao Yoshua aliuteketeza.
14Waisraeli wakatwaa vitu vyote walivyonyanganya na nyama wa miji hiyo; lakini waliwaua wakaaji wake wote, wala hawakumwacha hata mutu mumoja.
15Musa mutumishi wa Yawe aliipewa amri hii, naye Musa akamwamuru Yoshua ambaye aliitimiza. Yoshua alitimiza kila jambo Yawe alilomwamuru Musa.
Inchi Yoshua alizoteka16Yoshua aliiteka inchi nzima: sehemu za milima na sehemu zote za kusini, eneo lote la Goseni, inchi ya mabonde, inchi ya Araba, milima ya Israeli na sehemu zake za mabonde;
17aliwateka na kuwaua wafalme wote wa inchi hizo kuanzia kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki karibu na Seiri mpaka Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni, upande wa kusini wa mulima Hermoni.
18Vita Yoshua aliyopigana na wafalme hawa wote ilikamata muda murefu.
19Hakuna muji ambao ulifanya mapatano ya amani na Waisraeli, isipokuwa Gibeoni tu, ambamo Wahivi waliishi. Waisraeli waliiteka miji mingine yote kwa kupigana vita.
20Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.
21Wakati ule, Yoshua akakwenda, akawaangamiza Waanaki waliokuwa wanaishi katika milima kule Hebroni, Debiri, Anabu, inchi yote ya milima ya Yuda na Israeli. Yoshua akawaangamiza watu hao pamoja na miji yao.
22Hakuna mutu wa kabila la Anaki ambaye alibakia katika inchi ya Israeli; walibaki wachache tu katika miji ya Gaza, Gati na Asidodi.
23Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.