Hagai UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZITunavyoambiwa kwa mwanzo wa kitabu hiki, Hagai alihubiri kuanzia mwaka wa pili wa utawala wa Dario mufalme wa Persia, ni kusema katika mwaka wa 520 mbele ya Kristo, karibu miaka 20 nyuma ya Wayuda waliokuwa katika uhamisho kule Babeli kuruhusiwa na mufalme wa Persia kurudi kwao. Kundi la kwanza la Waisraeli lilirudi kwao kuanzia mwaka wa 538 mbele ya Kristo. Nyuma ya Wayuda kurudi kwao, walianza shuguli za kujenga upya hekalu lililoharibiwa na Wababeli katika mwaka wa 587. Lakini walikata tamaa; ndiyo maana nabii anawatia moyo waendelee. Anawatangazia kwamba, hekalu jipya litapendeza kuliko lile la kwanza (2.1-9) na kwamba ujenzi wake utamaliza hali ya uchafu na umasikini uliowapata watu wa Mungu (2.10-20). Hekalu inaitwa “Nyumba ya Yawe” katika kitabu hiki na katika vitabu vingi vingine.Kwa maneno ya Hagai ya kuwapa watu moyo, aliwahimiza watu wa nyakati zake wakuwe na bidii na kuifanya kazi wakitazamia hali mupya ambayo Mungu amewatayarishia.