Zaburi 45 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mashairi ya kumusifu mufalme

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo: “Mayungiyungi.” Mashairi ya Wakora. Wimbo wa mapenzi.

2Moyo wangu umejaa mawazo mazuri:

ninamutungia mufalme mashairi yangu,

ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.

3Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote,

maneno yako ni rehema tupu,

Mungu amekubariki milele.

4Ujifungie upanga wako, ewe shujaa!

Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.

5Songa mbele kwa utukufu upate ushindi,

utetee ukweli na kulinda haki.

Mukono wako utende mambo makubwa.

6Mishale yako ni mikali,

inapenya mioyo ya waadui za mufalme;

nayo mataifa yanaanguka chini yako.

7Kiti chako cha kifalme ni imara,

kinadumu milele kama cha Mungu.

Wewe unatawala watu wako kwa haki.

8Unapenda haki na kuchukia uovu.

Kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekupendelea kuliko wenzako;

amekuweka kuwa mufalme

kwa kukupakaa mafuta ya kufurahisha.

9Nguo zako zinanuka marasi, udi, na mudalasini;

muziki wa vinubi unakufurahisha katika nyumba ya pembe za tembo.

10Wabinti za wafalme ni kati ya wanaokupokea,

naye malkia amesimama kwa kuume kwako,

amevaa mapambo ya zahabu safi kabisa ya Ofiri.

11Sikiliza binti, ufikiri!

Tega sikio lako:

sahau sasa taifa lako na jamaa yako.

12Uzuri wako unavuta moyo wa mufalme;

yeye ni bwana yako, lazima umutii.

13Watu wa Tiro watakuletea zawadi;

watajiri watajipendekeza kwako.

14Binti wa mufalme anaingia, naye ni muzuri kabisa!

Nguo yake imefumwa na nyuzi za zahabu.

15Akiwa amevaa nguo za rangi nyingi,

anaongozwa kwa mufalme,

akisindikizwa na wabinti wenzake.

16Kwa furaha na shangwe wanafika huko,

na kuingia katika nyumba ya mufalme.

17Ee mufalme, utapata watoto wengi

watakaotawala pahali pa babu zako;

utawafanya watawale katika dunia yote.

18Nitalifanya jina lako litukuzwe katika vizazi vyote,

nayo mataifa yatakusifu milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help