1Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Ang. Isa 19.1-25; Yer 46.2-26; 29.6; Ang. Isa 36.6
2Wewe mwanadamu! Ugeuke kuelekea mufalme wa Misri, utoe unabii juu yake na juu ya inchi yote ya Misri.
3Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri,
wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili!
Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako,
kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
4Basi, nitakutia ndoana katika mataya yako,
na kuamuru samaki wakwame katika magamba yako.
Nitakuvua kutoka huko ndani ya muto.
5Nitakutupa katika jangwa,
wewe na samaki hao wote.
Mwili wako utaangukia katika mbuga;
wala hakuna atakayekuokota kusudi akuzike.
Nimeutoa mwili wako
ukuwe chakula cha nyama wakali na ndege.
6Halafu wakaaji wote wa Misri watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Waisraeli walikutegemea wewe ee Misri, lakini umekuwa zaifu kama utete.
7Walipokushika kwa mukono, ulivunjika na kutegua mabega yao. Walipokuegemea ulivunjika na kutetemesha viungo vyao.
8Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaleta upanga juu yako na kuwaua watu na nyama wako wote.
9Kwa sababu umesema kwamba muto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, inchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
10Hakika nitakuazibu wewe na mito yako; kwa hiyo nitaifanya inchi ya Misri kuwa jangwa na tupu toka Migidoli mpaka Sewene hata kwenye mipaka ya Etiopia.
11Hakuna mutu wala nyama atakayepita huko. Haitakaliwa kwa muda wa miaka makumi ine.
12Kati ya miji yote iliyoharibika, miji ya Misri itakuwa mitupu kwa miaka makumi ine. Nitawasambaza Wamisri kati ya watu wa mataifa mengine na kuwaeneza katika inchi zingine.
13Lakini Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kisha ile miaka makumi ine nitawakusanya Wamisri kutoka kwa mataifa walimosambazwa.
14Nitawafanikisha tena Wamisri. Nitawarudisha katika inchi ya Patro, inchi yao ya asili. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu,
15ufalme zaifu kuliko falme zote; wala hawataweza kujipandisha juu ya mataifa mengine. Nitawafanya Wamisri wakuwe watu zaifu hata wasiweze kuyatawala mataifa mengine tena.
16Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na Waisraeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea inchi ya Misri. Waisraeli watatambua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.
Mufalme Nebukadneza ataishinda Misri17Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mwaka wa makumi mbili na saba tangu tulipopelekwa katika uhamisho, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18Wewe mwanadamu! Nebukadneza, mufalme wa Babeli, aliwalazimisha waaskari wake kufanya kazi ngumu ya kuishambulia Tiro. Vichwa vyote vya waaskari wake vilipata upaa na mabega yote yalichubuka. Lakini yeye, wala waaskari wake, hawakupata chochote kutokana na kazi hiyo aliyoifanya juu ya Tiro.
19Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitamupa Nebukadneza mufalme wa Babeli, inchi ya Misri. Atanyanganya mali yake yote, na kutwaa utajiri wa Misri kuwa mushahara wa waaskari wake.
20Nimemupa inchi ya Misri kuwa mushahara wa jasho lake kwa maana waaskari wake walifanya kazi kwa ajili yangu.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
21Siku hiyo, nitawafanya Waisraeli wakuwe na nguvu na kukuwezesha wewe Ezekieli useme kati yao. Nao watapata kujua kwamba mimi ni Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.