Zaburi 42 - Swahili Congo Revised Bible 2002

SEHEMU YA PILI(Zaburi 42–72)Maombi ya mukimbizi

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.

2Kama pongo anavyotamani maji ya kijito,

ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!

3Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima.

Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?

4Machozi ni chakula changu muchana na usiku;

ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”

5Katika huzuni yangu, ninakumbuka

jinsi nilivyokwenda na kundi la watu

na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu

wakipiga vigelegele vya shukrani,

kundi la watu likifanya sherehe!

6Mbona ninaugua hivyo katika moyo?

Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu?

Nitamutumainia Mungu,

maana nitamusifu tena

yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

7Roho yangu imeregea kabisa,

kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,

kutoka katika eneo la Yordani,

kutoka mulima Hermoni na Mizari.

8Mafuriko juu ya mafuriko yananguruma,

mawimbi na zoruba yako vinanifunika.

9Yawe atanijalia wema wake muchana;

nami nitamwimbia wimbo wa sifa usiku,

nitamwomba Mungu anayenipa uzima.

10Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu:

“Kwa nini umenisahau?

Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza

kwa kuteswa na adui yangu?”

11Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao,

wanaponiuliza kila siku:

“Mungu wako, yupo wapi?”

12Mbona ninaugua hivyo katika moyo?

Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu?

Nitamutumainia Mungu,

maana nitamusifu tena Mungu,

anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help