Isaya 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Wakati huo wanawake saba watashikamana na mwanaume mumoja na kumwambia: Chakula na mavazi tutajitafutia wenyewe, lakini wewe utuondolee haya yetu, uturuhusu tuitwe kwa jina lako.

Muji Yerusalema utabarikiwa tena

2Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.

3Wale watakaobaki wazima katika Yerusalema, huko Sayuni, wataitwa Wachaguliwa wa Mungu; hao ndio wale wote watakaokuwa wameandikwa katika kitabu chake waishi huko Yerusalema.

4Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.

5Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote. Ang. Kut 13.21; 24.16

6Utukufu wake utakuwa kwao kivuli kwa kuwakinga na joto la muchana; na kimbilio na kikingio chao wakati wa zoruba na mvua.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help