1“Wakati Yawe, Mungu wenu, atakapoteketeza watu wale ambao anawapa ninyi inchi yao, na kisha kuitwaa na kuishi katika nyumba zao,
2mutatenga miji mitatu katika inchi Yawe, Mungu wenu atakayowapatia muirizi.
3Mutatengeneza barabara na kugawanya katika sehemu tatu inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia muirizi kusudi yeyote anayemwua mutu bila kukusudia apate kukimbilia huko.
4“Mutu kwa bahati mbaya akimwua mwenzake bila kukusudia ambaye kwanza hakuwa adui yake,
5kwa mufano, mutu anayekwenda na mwenzake katika pori kukata kuni naye wakati anakata muti, shoka likachomoka kutoka kwenye mupini wake, na kumwua yule mwingine, mutu huyo anaweza kukimbilia kwenye muji mumoja, kwa kuokoa maisha yake.
6Lakini kama umbali wa muji huo ni mukubwa sana, huyo mwenye kulipiza kisasi, kwa hasira kali anaweza kumufuatilia, akimukamata na kumwua huyo aliyesababisha kifo, ingawa hakupewa hukumu ya kifo na hao wawili hawakukuwa waadui mbele.
7Kwa hiyo mimi ninawaamuru mutenge miji mitatu.
8“Tena kama vile Yawe, Mungu wenu, akipanua mipaka ya inchi yenu, kama vile alivyowaapia babu zenu, naye akiwapatia inchi yote ambayo aliahidi kuwapatia hao babu zenu
9ikiwa mutakuwa waangalifu kushika amri hizi zote, ninazowaamuru hivi leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata siku zote njia zake, basi, mutaongeza miji mingine mitatu zaidi ya hii mitatu,
10kusudi mutu asiyekuwa na kosa asiuawe katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia kuwa yenu, na hivyo kuwasababisha kuwa na kosa la mauaji.
11“Lakini mutu akiwa adui wa mwenzake, akivizia, akimushambulia na kumwua, kisha anakimbilia kwenye muji mumoja wa miji hiyo,
12hapo wazee wa muji huo watatuma watu wamutoshe kule na kumutoa kwa mwenye kulipiza kisasi cha umwangaji wa damu, auawe.
13Musimwonee huruma, lakini mutakomesha uovu wa mauaji ya mutu asiyekuwa na kosa katika Israeli, kusudi mupate kuishi kwa amani.
Mipaka ya zamani14“Musiondoe kitambulisho cha mipaka ya wajirani zenu, ambayo iliwekwa hapo zamani katika inchi ambayo Yawe wenu anawapatia muirizi.
Washuhuda15“Ushuhuda wa mutu mumoja hautoshi kwa kuhukumu mutu juu ya kosa lolote au uovu juu ya kosa lolote alilofanya. Ni ushuhuda wa watu wawili au watatu tu ndio utakaohakishwa.
16Ikiwa mushuhuda wa uongo atatokea kwa kumushitaki mutu yeyote juu ya kosa fulani,
17basi hao wote wawili wanaobishana watakwenda mbele ya Yawe, mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako katika kazi wakati huo.
18Waamuzi watachunguza kwa uangalifu maneno hayo na ikiwa mushuhuda ni mushuhuda wa uongo na amemushitaki mwenzake kwa uongo,
19basi, mutamutendea sawa vile alivyokusudia kumutendea ndugu yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
20Nao watu wengine watasikia na kuogopa, na uovu kama huo hautafanyika tena kati yenu.
21Musiwaonee huruma watu wa aina hiyo. Uzima utalipwa kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono na muguu kwa muguu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.