Zefania 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hukumu ya Yerusalema

1Ole wake Yerusalema,

muji wa uasi, muchafu, na wenye kujaa watesaji.

2Hausikilizi onyo lolote,

wala haukubali kutii.

Haukumutegemea Yawe hata kidogo,

wala kumukaribia Mungu wake.

3Wakubwa wake ni simba wanaonguruma,

waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi

wasioacha chochote mpaka asubui.

4Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu.

Makuhani wake wamevichafua vitu vitakatifu

na kuivunja sheria kwa nguvu.

5Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki,

yeye hatendi jambo lolote baya.

Kila siku asubui anatangaza hukumu yake,

kila kunapopambazuka anaitimiza.

Lakini waovu hawana haya hata kidogo.

6Yawe anasema:

Nimeyateketeza kabisa mataifa;

kuta zao za kujikinga ni mabomoko.

Barabara zao nimeziharibu,

na hakuna anayepita ndani yake.

Miji yao imekuwa mitupu,

bila watu, na bila wakaaji.

7Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii

na kukubali kuonywa;

hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu.

Lakini watu wake walizidisha tamaa zao

za kufanya matendo yao kuwa upotovu.

8Kwa hiyo muningojee mimi Yawe,

ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki.

Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme,

kuyamwangia kasirani yangu,

na ukali wa hasira yangu.

Dunia yote itateketezwa

kwa moto wa kasirani yangu.

9Wakati huo nitabadilisha luga ya watu,

nitawawezesha kusema luga safi

kusudi waniite mimi Yawe,

na kuniabudu kwa moyo mumoja.

10Kutoka ngambo ya mito ya Kushi

watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika,

wataniletea sadaka yangu.

11Siku hiyo, hautapata haya

kutokana na matendo yako ya kuniasi,

maana nitawaondoa kati yako

wale wanaojivuna na kujitukuza,

nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.

12Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu

ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.

13Waisraeli watakaobaki

hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo,

wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote.

Watapata chakula na kulala

wala hakuna mutu atakayewaogopesha.

Wimbo wa furaha

14Imba kwa sauti, ewe Sayuni,

piga vigelegele, ee Israeli.

Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalema!

15Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako,

amewafukuza waadui zako.

Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe.

Hautaogopa tena hasara.

16Siku hiyo, Yerusalema utaambiwa:

Usiogope, ee Sayuni,

usilegee mikono.

17Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe.

Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi.

Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa.

Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya.

Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,

18kama vile katika siku ya sikukuu.

Yawe anasema:

Nitakuondolea hasara zako,

nawe hautahitaji kupata haya kwa ajili yake.

19Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza.

Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa

na kubadilisha haya yao kuwa sifa

na utukufu katika dunia yote.

20Wakati huo nitawakusanya,

na kuwafanya mujulikane na kusifiwa

kati ya watu wote katika dunia,

na kuwarudishia hali yenu njema,

nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe.

–Ni Yawe anayesema hivyo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help