1Yawe akamwambia Musa:
2Uwaambie watu wa Israeli hivi: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
3Musifanye kama vile watu wa inchi ya Misri ambako mulikaa wanavyofanya, wala musifanye kama vile watu wa inchi ya Kanana ambako ninawapeleka wanavyofanya. Musifuate desturi zao hata kidogo.
4Ninyi mutafuata maagizo yangu na kushika masharti yangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
5Munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu: yule anayeyashika ataishi. Mimi ni Yawe.
6Mutu yeyote wa Israeli haruhusiwi kumukaribia mwanamuke wa jamaa yake wa karibu kusudi alale naye. Mimi ni Yawe.
7Usimuvunjie heshima baba yako kwa kulala na mama yako aliyekuzaa. Usimupatishe haya, yeye ni mama yako.
8Usimuvunjie heshima baba yako kwa kulala na mumoja wa wake zake. Hao ni wamama zako.
9Usilale na dada yako, akuwe ni dada yako, binti wa baba yako au wa mama yako hata kama alizaliwa katika nyumba au pahali pengine.
10Usilale na mujukuu wako, mutoto wa mwana wako au binti yako, maana sehemu zao za siri ni kama zako mwenyewe.
11Usilale na binti aliyezaliwa na muke wa baba yako aliyeolewa na baba yako. Binti huyo ni dada yako.
12Usilale na shangazi yako, maana huyo ni dada ya baba yako.
13Usilale na dada ya mama yako, maana huyo ni mama yako mukubwa au mudogo.
14Usilale na muke wa baba yako mukubwa au mudogo; huyo ni mama yako.
15Usilale na muke wa mwana wako, huyo ni muke wa mwana wako. Usilale naye.
16Usilale na muke wa ndugu yako, huyo ni shemeki yako.
17Ukilala na mwanamuke, basi, usilale naye na binti yake, wala wajukuu zake. Hao ni wandugu. Kuwachanganya ni kufanya uovu.
18Usimwoe dada ya muke wako wakati muke wako angali anaishi, hiyo itasababisha mapigano.
19Usilale na mwanamuke anapokuwa na ugonjwa wa mwezi.
21Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.
22Usilale na mwanaume mwenzako kama vile ni mwanamuke. Hilo ni chukizo.
24Musijichafue kwa kufanya mambo hayo maana kwa sababu ya mambo hayo ninafukuza mataifa yanayokuwa mbele yenu kwa vile wao wanafanya hayo na kujichafua.
25Inchi yao ilichafuliwa nami nikaiazibu, nayo ikawakataa wakaaji wake.
26Lakini ninyi na wageni wanaokaa kati yenu munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu na wala musifanye machukizo hayo.
27Machukizo hayo yalifanywa na watu waliokaa katika inchi ya Kanana mbele yenu, nao wakachafua inchi.
28Basi, ninyi musifanye mambo hayo, kama sivyo inchi hiyo itawatapika kama vile ilivyolitapika taifa lililokuwa mbele yenu.
29Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza wanapaswa kutengwa mbali na watu wao.
30Kwa hiyo mushike kwa ukamilifu yote ninayowaagiza. Musifuate tabia zozote ya kuchukiza zilizofanywa na wale walioishi katika inchi mbele yenu, kusudi musijichafue kwa njia yake. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.