1Wandugu, tunapenda kuwajulisha namna Mungu alivyojalia neema makanisa ya Makedonia.
2Yalijaribiwa sana kwa njia ya mateso mengi yaliyopata. Lakini yalizidi kuwa na furaha hata yakakuwa na moyo wa kutoa kupita kipimo, ingawa yalikuwa masikini sana.
3Ninayashuhudia kwamba kwa mapenzi yao yalitoa kwa kadiri yalivyoweza na hata zaidi kupita uwezo wao.
4Yalitusihi sana tukishiriki nayo katika kazi ya kuwasaidia watu wa Mungu wanaokaa Yudea.
5Yalitoa kupita vile tulivyokuwa tukitumaini! Kwanza yalijitoa yenyewe kwa ajili ya kazi ya Bwana, kisha yakajitoa kwa ajili yetu vilevile kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6Ni kwa hiyo tulimusihi Tito atimize kazi hiyo ya kuwaongoza ninyi kuwa na moyo wa kutoa sawa alivyoianzisha.
7Ninyi munakuwa na kila kitu kwa uwingi: imani, usemi, ufahamu, kuwa na bidii ya kila namna na upendo munaokuwa nao kwetu. Kufuatana na hiyo mukuwe vilevile na uwingi katika kazi hii ya kuwa na moyo wa kutoa.
8Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.
9Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.
10Kuelekea jambo hilo, mimi ninawatolea shauri, nalo linafaa kwenu, kwa maana ni ninyi muliokuwa wa kwanza kukusudia kufanya kazi ile na kuianzisha tangu mwaka jana.
11Sasa muendelee nayo na kuitimiza. Kama vile mulivyokuwa na moyo mwema wa kukusudia kuifanya, basi mukuwe na moyo mwema wa kuitimiza kufuatana na uwezo wa mali munayokuwa nayo.
12Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.
13Nia yangu si kusema kwamba munapaswa kujitia katika taabu kwa ajili ya kusaidia watu wengine, lakini inafaa kuwe usawa.
14Na sasa ninyi muko na mapato mengi zaidi, basi munaweza kuwasaidia wale wanaokuwa katika mahitaji. Hivi wao vilevile watakapokuwa na mapato mengi wataweza kuwasaidia katika siku za mahitaji. Kwa hiyo kutakuwa usawa
15kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema:
“Yule aliyeokota kingi hakukuwa na cha zaidi,
na aliyeokota kidogo, hakupungukiwa.”
Tito na wenzake16Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!
17Amekubali ombi letu, na zaidi ya ile ameondoka kuja huko kwenu kwa bidii yake kubwa na kutokana na mapenzi yake mwenyewe.
18Pamoja naye tunamutuma ndugu anayesifiwa na makanisa yote kwa ajili ya kazi yake ya kuhubiri Habari Njema.
19Vilevile, yule ndugu amechaguliwa na makanisa kwa kutusindikiza katika safari ya kutimiza kazi hii ya kutoa kwa moyo mwema ambayo sisi tunafanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana, na kwa kuonyesha nia yetu ya kusaidia watu wengine.
20Tunaepuka kushitakiwa na watu wengine juu ya mali mingi kama hii tunayochunga.
21Kwa maana tunataka kufanya mema, si mbele ya Bwana tu, lakini mbele ya watu vilevile.
22Tunatuma ndugu yetu mwingine pamoja nao. Sisi tumemupima mara nyingi na ameonyesha siku zote kwamba yeye ni mwenye bidii sana. Na sasa, yeye ni mwenye bidii zaidi tena kwa kuwa anawaaminia ninyi sana.
23Kwa ngambo ya Tito, yeye ni mwenzangu, ninafanya kazi pamoja naye kwa ajili yenu. Nao wale wandugu wengine wanaomusindikiza, ni wajumbe wa makanisa wanaotumika kwa ajili ya utukufu wa Kristo.
24Kwa hiyo muonyeshe mbele ya makanisa kwamba hakika munawapenda na kuyafahamisha kwamba tulikuwa na haki ya kujivuna kwa ajili yenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.