1Mashairi ya Asafu.
Kwa nini,
ee Mungu,
umetutupilia kabisa?
Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako?
2Kumbuka taifa lako ulilojipatia tangia zamani,
kabila ulilokomboa likuwe mali yako.
Kumbuka mulima Sayuni pahali unapokaa.
3Pita juu ya mabomoko haya ya tangu zamani!
Waadui wameharibu kila kitu katika hekalu.
4Waadui zako wamepiga kelele la ushindi katika hekalu lako!
Wamesimika humo bendera zao za ushindi!
5Wanafanana na mukataji wa kuni,
anayekata miti kwa shoka lake.
6Walivunjavunja michoro ya hekalu,
kwa mashoka na nyundo zao.
7Waliunguza pahali patakatifu pako;
walikufuru pahali pale unapoheshimiwa.
8Walikusudia kutuangamiza wote pamoja;
walichoma pahali pote katika inchi
ambapo tulikutana kwa kukuabudu.
9Hatuoni tena vitambulisho vya kuwa kwako kati yetu,
hatuna tena nabii yeyote,
wala hakuna anayejua mwisho wa haya yote!
10Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea?
Watakufuru jina lako milele?
11Mbona umeficha mukono wako wa kuume?
Kwa nini haunyooshi mukono na kuwapiga?
12Hata hivyo wewe Mungu ni mufalme wetu tangu zamani;
umefanya mambo makubwa ya kuokoa katika inchi.
13Kwa uwezo wako mukubwa uligawanya bahari;
uliponda vichwa vya nyama mukubwa wa bahari.
14Wewe uliponda vichwa vya nyama mukubwa Leviatani;
ukawapa wanyama wa jangwa muzoga wake.
15Wewe umefanya chemichemi na vijito;
na kukausha mito mikubwa.
16Muchana ni wako na usiku ni wako;
umeweka mwezi na jua kwenye nafasi zao.
17Wewe umeweka mipaka yote ya dunia;
umepanga wakati wa kipwa na wakati wa mvua.
18Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako;
taifa pumbafu linatukana jina lako.
19Usitutupie, sisi njiwa wako, kwa wanyama wakali,
usisahau kwa siku zote maisha ya wamasikini wako.
20Ukumbuke agano ulilofanya nasi!
Inchi imejaa mateso makali kila nafasi za giza.
21Usiwaache wanaogandamizwa wafezeheshwe,
uwajalie wamasikini na wakosefu wasifu jina lako.
22Ee Mungu, simama sasa ujitetee!
Ukumbuke mazarau ya kila siku ya wasiokujua.
23Usisahau makelele ya waadui zako;
na fujo ya siku zote ya wapinzani wako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.