1“Mwanaume yeyote asilale na muke wa baba yake.
Kutengwa na watu wa Mungu2“Mwanaume yeyote aliyeumizwa au aliyekatwa kiungo chake cha kiume haruhusiwi kujiunga na kusanyiko la watu wa Yawe.
3“Na mwana haramu yeyote, wala muzao wake hata kizazi cha kumi, haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.
4“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,
5kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.
6Lakini Yawe, Mungu wenu, hakumusikiliza Balamu; pahali pake laana hiyo iligeuka kuwa baraka, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, aliwapenda.
7Kwa hiyo, musiwasaidie hao hata kidogo kusudi wapate amani na fanaka.
8“Musiwachukie Waedomu; hao ni wandugu zenu. Na musiwachukie Wamisri, maana mulikaa katika inchi yao kama vile wageni.
9Wazao wao, kuanzia kizazi cha tatu, wataruhusiwa kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.
Usafi katika kambi10“Mukienda kwa vita, mukipiga kambi, kila mumoja afanye angalisho na kitu chochote kiovu.
11Kama kati yenu kuna mutu yeyote ambaye ni muchafu kwa sababu ya kutokwa mbegu usiku, huyo atatoka inje ya kambi; hatakaa karibu na kambi.
12Lakini ikifika magaribi ataoga, na jua likitua anaweza kurudi katika kambi.
13“Munapaswa kuwa na pahali inje ya kambi ambapo munaweza kwenda kwa choo.
14Kati ya vifaa vyenu mutakuwa na jembe, na hilo mutalitumia kuchimba shimo na kufukia mavi yenu.
15Kambi yenu inapaswa kuwa takatifu kwa sababu Yawe, Mungu wenu anatembea katika kambi yenu kusudi awaokoe na kuwatia waadui zenu katika mikono yenu. Kwa hiyo musimwache aone kitu chochote kisichofaa kati yenu, kama sivyo atawaacha ninyi.
16“Mutumwa akikimbilia kwako usimurudishe kwa bwana wake.
17Ataishi pamoja nawe pahali atakapochagua katika moja ya makao yako, pahali panapomupendeza. Usimutese.
18“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.
19Feza yoyote iliyopatikana na vitendo vya ukahaba huo, isipelekwe ndani ya hekalu la Yawe, Mungu wenu, kwa kulipia kiapo, maana mwanaume au mwanamuke anayekuwa kahaba wa kidini ni chukizo kwa Yawe.
20“Usimukopeshe ndugu yako Mwisraeli kitu kwa faida; usimulipishe faida juu ya mukopo wa feza, chakula, au chochote ambacho watu wanakopesha kwa faida.
21Unaweza kuomba faida unapomukopesha mugeni, lakini ndugu yako Mwisraeli usimulipishe faida, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki katika shuguli zako zote utakazofanya katika inchi ambayo unakwenda kurizi.
22Unapofanya kiapo mbele ya Yawe, Mungu wako, usichelewe kukitimiza, maana Yawe, Mungu wako, atakidai kwako, nawe utakuwa na kosa.
23Lakini ukiacha kufanya kiapo hautakuwa na zambi.
24Ukuwe mwangalifu kutimiza kiapo ulichosema kwa mudomo wako, maana ulimwahidi Yawe, Mungu wako, kwa mapenzi yako.
25“Ukipitia katika shamba la muzabibu la mwenzako unaweza kula zabibu kadiri unavyoweza, lakini usichume na kupeleka zabibu zozote katika kikapu chako.
26Ukipitia katika shamba la mwenzako lenye ngano unaweza kukwanyua masuke kwa mukono na kula, lakini usitwae kisu kwa kukata mazao yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.