1Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala miaka makumi tatu na mumoja akiwa kule Yerusalema. na watu wengine wote wakubwa kwa wadogo. Halafu akawasomea maneno ya kitabu cha agano kilichopatikana katika nyumba ya Yawe.
31Kisha mufalme akasimama kwa pahali pake akafanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri, maamuzi na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
32Tena akawasukuma wote waliokuwa katika Yerusalema na inchi ya Benjamina kushika agano lile. Nao wakaaji wa Yerusalema walitenda kwa kufuata agano la Mungu, Mungu wa babu zao.
33Kisha Yosia akaondoa sanamu zote za kuchukiza zilizokuwa katika eneo lote la watu wa Israeli, na kuwasukuma watu wote wa Israeli kumutumikia Yawe, Mungu wao. Katika maisha yake yote hawakumwacha Yawe, Mungu wa babu zao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.