Kutoka 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mutoto Musa anaokotwa katika muto Nili

1Kulikuwa mutu mumoja wa ukoo wa Walawi aliyemuoa mwanamuke mumoja ambaye vilevile alikuwa wa ukoo wa Walawi.

2Basi, mwanamuke yule akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Alipoona kwamba mutoto yule muchanga alikuwa muzuri, akamuficha kwa muda wa miezi mitatu. akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani.

4Dada ya yule mutoto akajificha karibu na pahali pale kusudi aone yatakayomupata ndugu yake.

5Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae.

6Alipokifungua, akamwona yule mutoto muchanga akilia. Basi, akamwonea huruma, akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.”

7Palepale dada ya yule mutoto akajitokeza, akamwambia binti ya mufalme: “Niende nikutafutie yaya kati ya wanawake Waebrania akulelee mutoto huyu?”

8Binti ya mufalme akamwambia: “Kwenda.” Basi, yule binti akaenda, akamwita mama ya yule mutoto.

9Binti ya mufalme akamwambia yule mama: “Utunze mutoto huyu, umulee kwa ajili yangu, nami nitakulipa mushahara wako.” Basi, yule mama akamutwaa mutoto, akamulea.

10Mutoto alipokuwa mukubwa, mama yake akamupeleka kwa binti ya mufalme, naye akamutwaa na kumufanya mwana wake. Binti ya mufalme akasema: “Nimemutoa ndani ya maji,” kwa hiyo akamupa mutoto yule jina Musa.Musa anakimbilia Midiani

11Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.

Siku moja, Musa alikuwa akikaa kando ya kisima cha maji. Kilio cha Waisraeli katika utumwa

23Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.

24Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.

25Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help