1Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa,
ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,
2utaweza kumwambia Yawe:
“Wewe ni kimbilio langu ninamojificha,
Mungu wangu ninayemutumainia!”
3Hakika Mungu atakuokoa katika mutego,
atakukinga na magonjwa mabaya.
4Atakufunika kwa mabawa yake;
utapata usalama kwake.
Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.
5Hautaogopa vitisho vya usiku,
wala shambulio la rafla muchana.
6Hautaogopa ugonjwa mukali unaotokea usiku,
wala hasara inayotokea muchana.
7Kama watu elfu wakianguka pembeni yako,
hata elfu kumi karibu yako,
hasara haitakupata.
8Kwa macho yako mwenyewe utaangalia,
na kuona jinsi watu waovu wanavyoazibiwa.
9Wewe umemufanya Yawe kuwa kimbilio lako;
Mungu anayekuwa juu kuwa tegemeo lako.
10Kwa hiyo, hautapatwa na hasara yoyote;
nyumba yako haitakaribiwa na pigo lolote.
11Maana Mungu atawaamuru wamalaika wake,
wakulinde popote unapoenda.
12Watakuchukua katika mikono yao,
kusudi usijikwae kwenye jiwe.
13Utakanyaga simba na nyoka wa hatari,
utawaponda simba wakali na nyoka.
14Mungu anasema: “Nitamwokoa yule anayenipenda;
nitamulinda anayejua jina langu!
15Akiniita, mimi nitamwitikia;
akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye,
nitamwokoa na kumupa heshima.
16Nitamupa maisha marefu,
nitamujalia wokovu wangu.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.