1Ilipokuwa kwa mwanzo wa mwaka mupya, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Daudi alimutuma Yoabu na wakubwa wake pamoja na waaskari wote wa Israeli kupigana. Nao waliteka Waamoni na kushambulia muji wa Raba. Lakini Daudi alibaki Yerusalema.
2Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.
3Daudi akatuma mutu kuuliza mwanamuke yule ni nani. Mutu yule akamwambia Daudi: “Mwanamuke yule ni Batiseba binti ya Eliabu, na muke wa Uria wa Hiti.”
4Basi, Daudi alituma wajumbe wamulete. Basi Batiseba akakuja kwa Daudi, naye Daudi akalala naye. Kisha akarudi kwake. Mwanamuke yule alikuwa akitoka kujitakasa kisha ugonjwa wake wa mwezi.
5Mwanamuke yule akapata mimba, naye akatuma habari kwa Daudi kwamba yuko na mimba yake.
6Basi, Daudi akamutumia Yoabu ujumbe: “Umutume Uria wa Hiti kwangu.” Naye Yoabu akamutuma Uria kwa Daudi.
7Uria alipofika kwake, Daudi alimwuliza habari za Yoabu, watu wote, na hali ya vita.
8Halafu Daudi alimwambia Uria: “Urudie kwako unawe miguu yako.” Uria alitoka kwa mufalme, na mara moja mufalme akamupelekea zawadi.
9Lakini Uria hakurudi kwake. Alilala pamoja na watumishi wote wa bwana wake kwenye mulango wa nyumba ya kifalme.
10Daudi aliposikia kwamba Uria hakwenda kwake, Daudi akamwuliza Uria: “Wewe umetoka safari, kwa nini haukuenda kwako?”
11Uria alimujibu Daudi: “Sanduku la Agano, pamoja na waaskari wote wa Israeli na Yuda wanakaa kwenye vibanda katika vita. Bwana wangu Yoabu na watumishi wake wote wamepiga kambi katika mbuga. Basi ni vizuri mimi niende nikule na kunywa na kulala na muke wangu? Ninaapa kwamba, kama vile unavyoishi, sitafanya kitu cha namna ile.”
12Kisha, Daudi akamwambia Uria: “Basi, ukae hapa leo tena, na kesho nitakuacha urudie.”
Kwa hiyo Uria akabaki katika muji wa Yerusalema siku hiyo. Siku iliyofuata,
13Daudi alimwalika Uria kula na kunywa kule kwake, akamulewesha Uria. Hata hivyo, usiku ule Uria hakwenda kwake, lakini alilala kwenye kilalio chake pamoja na watumishi wa bwana wake.
14Asubui yake, Daudi alimwandikia Yoabu barua, akamupa Uria aipeleke kwa Yoabu.
15Katika barua hiyo Daudi aliandika hivi: “Umuweke Uria kwenye mustari wa mbele, pahali ambako mapigano ni makali kabisa, kisha umwache kule na kurudia nyuma kusudi apigwe, na akufe.”
16Basi, Yoabu alipokuwa akizunguka muji, alimuweka Uria pahali ambapo alijua wazi waaskari wa waadui walikuwa hodari sana.
17Wakaaji wa muji ule walitoka katika muji wao na kupigana na Yoabu. Watumishi wamoja wa Daudi, waliuawa. Uria wa Hiti naye aliuawa vilevile.
18Kisha, Yoabu alipeleka habari zote kwa Daudi akimwelezea juu ya vita.
19Yoabu akamwamuru huyo mutumishi aliyemutuma hivi: “Kisha kumwelezea mufalme mambo yote juu ya vita,
20naye akikasirika na kukuuliza: ‘Kwa nini mulikwenda karibu na muji mulipokuwa munapigana? Hamukujua kwamba wangewapiga mishale kutoka kwenye kuta za muji wao?
21Nani alimwua Abimeleki mwana wa Yerubeseti? Si alikuwa mwanamuke mumoja katika muji wa Tebesi ambaye alitupa jiwe la kusagia kutoka kwenye ukuta nalo likamwua Abimeleki? Kwa nini basi, mulikwenda karibu na ukuta?’ Basi, wewe utamwambia hivi: ‘Hata mutumishi wako Uria wa Hiti, naye amekufa.’ ”
22Yule mujumbe alikwenda kwa Daudi na kumwambia yote ambayo aliyotumwa na Yoabu ayaseme.
23Yule mujumbe akamwambia Daudi: “Waadui zetu walitushinda nguvu, wakatoka inje ya miji na kutushambulia katika mbuga. Hata hivyo sisi tuliwarudisha mpaka kwenye mulango wa muji.
24Halafu wakatupiga mishale sisi watumishi wako kutoka juu ya ukuta. Watumishi wako wamoja waliuawa. Hata mutumishi wako Uria wa Hiti, naye amekufa.”
25Daudi akamwambia yule mujumbe: “Utamwambia Yoabu hivi: ‘Jambo hili lisikusumbue maana upanga hauna macho, vita inaua haizuru nani. Lakini, imarisha mashambulizi juu ya muji, mpaka uangamize muji ule’. Ndivyo utakavyomutia Yoabu moyo.”
26Batiseba muke wa Uria aliposikia kwamba mume wake Uria amekufa, akafanya kilio kwa ajili yake.
27Muda wa kufunga kilio ulipokwisha, Daudi aliagiza wamulete Batiseba na kumupeleka katika nyumba yake. Batiseba akakuwa muke wa Daudi, naye akamuzalia Daudi mutoto mwanaume. Lakini jambo hilo Daudi alilofanya lilimuchukiza Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.