1Nyuma ya kufa kwa Saulo, Daudi alirudi kisha kuwashinda Waamaleki, akakaa Ziklagi kwa muda wa siku mbili.
2Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.
3Daudi akamwambia: “Unatoka wapi?”
Naye akamwambia: “Nimetoroka kutoka katika kambi ya Waisraeli.”
4Daudi akamwambia: “Uniambie jinsi mambo yalivyokuwa kule.”
Yule mutu akamujibu: “Watu wetu wameyakimbia mapigano na wengi kati yetu wameuawa. Zaidi ya hayo, Saulo na mwana wake Yonatani vile vile wameuawa.”
5Daudi akamwuliza yule kijana: “Unajua namna gani kwamba Saulo na mwana wake Yonatani wamekufa?”
6Yule kijana akamujibu: “Kwa bahati, nilikuwa juu ya mulima Gilboa. Nilimwona Saulo akiegemea mukuki wake na magari ya waaskari wapanda-farasi ya waadui zake yalikuwa yanamusonga sana.
7Saulo alipoangalia nyuma, aliniona, akaniita. Nilipoitika,
8yeye aliniuliza mimi ni nani, nami nikamwambia kwamba mimi ni Mwamaleki.
9Kwa hiyo, akaniambia: ‘Sogea karibu uniue maana nimeumizwa vibaya na maumivu ni makali. Lakini ningali bado muzima’.
10Kwa hiyo, nilikwenda karibu naye na kumwua, kwa sababu nilikuwa na uhakika kwamba akianguka chini, hataweza kuishi zaidi. Lakini taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikomo kilichokuwa kwenye mukono wake, vyote nimekuletea wewe, bwana wangu.”
11Daudi akapasua nguo yake kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vilevile.
12Wakaomboleza, wakalia na kufunga kula mpaka magaribi kwa ajili ya Saulo, Yonatani mwana wake, na inchi ya Waisraeli, watu wa Yawe, kwa maana wengi kati yao waliuawa katika vita.
13Daudi akamwuliza yule kijana aliyemupasha habari: “Unatoka wapi?”
Yeye akajibu: “Mimi ni Mwamaleki, lakini ninaishi katika inchi yako kama mugeni.”
14Daudi akamwuliza: “Ilikuwa namna gani wewe haukuogopa kuunyoosha mukono wako na kumwua muchaguliwa wa Yawe?”
15Kisha, Daudi akamwita mumoja kati ya vijana wake akamwambia: “Umwue mutu huyu!” Yule kijana alimupiga yule Mwamaleki, naye akakufa.
16Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”
Daudi anaomboleza kifo cha Saulo na Yonatani17Daudi aliimba maombolezo haya kwa ajili ya Saulo na mwana wake Yonatani.
18Daudi alisema watu wa Yuda wafundishwe maombolezo hayo, nayo yameandikwa katika kitabu cha Yaseri. Daudi aliimba:
19Ewe Israeli,
utukufu wako umeuawa,
juu ya milima yako.
Angalia jinsi mashujaa walivyoanguka!
20Musiuambie muji wa Gati jambo lile
wala katika barabara za Askeloni,
kusudi wanawake wa Wafilistini wasishangilie,
wabinti za wapagani wasifurahi.
21Enyi milima ya Gilboa,
musikuwe na umande au mvua juu yenu.
Wala mashamba yenu yasitoe chochote siku zote.
Maana kule ngao za shujaa zilichafuliwa,
ngao ya Saulo haikupakaliwa mafuta.
22Upinde wa Yonatani haukurudi nyuma hata kidogo,
upanga wa Saulo haukurudi bure hata kidogo.
Viliua wengi siku zote,
Viliua mashujaa.
23Saulo na Yonatani,
watu wema na wa kupendeza.
Katika maisha na kifo hawakutengana.
Walikuwa wepesi kuliko tai,
wenye nguvu kuliko simba.
24Wanawake wa Israeli, mumulilie Saulo,
aliyewavalisha nguo nyekundu za utukufu,
aliyepamba nguo zenu kwa zahabu.
25Jinsi gani mashujaa walivyoanguka
katika vita.
Yonatani analala,
akiwa ameuawa kwenye milima.
26Ninasikitika kwa ajili yako, ndugu yangu Yonatani.
Umekuwa kwangu mutu wa kupendeza siku zote.
Pendo lako kwangu limekuwa la ajabu,
la ajabu kuliko la mwanamuke.
27Jinsi gani mashujaa walivyoanguka,
na silaha za vita zimeangamia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.