Yeremia 23 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ahadi ya kuwarudisha Waisraeli katika inchi yao

1Ole kwa wachungaji wanaowaangamiza na kusambaza kundi langu la kondoo!

–Ni ujumbe wa Yawe.

2Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: Ninyi munasambaza kondoo wangu na kuwafukuza, wala hamukuwatunza. Basi, nami vilevile nitawaazibu kwa ajili ya matendo yenu maovu.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

3Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.

4Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea.

–Ni ujumbe wa Yawe.

5Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.

6Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.

7Kwa hiyo, siku zinakuja siku ambapo watu hawataapa tena, wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa watu wa Israeli kutoka katika inchi ya Misri.

8Lakini wataapa wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa na kuwaongoza Waisraeli kutoka inchi ya kaskazini na kutoka inchi zote ambapo alipowafukuza. Na halafu wataishi katika inchi yao wenyewe.

–Ni ujumbe wa Yawe.

Manabii wabaya

9Ujumbe juu ya manabii wasiofaa.

Nimevunjika moyo,

mifupa yangu yote inatetemeka;

nimekuwa kama mulevi,

kama mutu anayetabanika na pombe,

kwa sababu ya Yawe

na maneno yake matakatifu.

10Maana, inchi imejaa wazinzi.

Kwa sababu ya laana, inchi inaomboleza,

na mashamba ya kulishia nyama yamekauka.

Mienendo ya watu ni miovu,

wanapoteza nguvu kwa ajili ya mambo yasiokuwa ya haki.

11Manabii na makuhani, wote hawamwogopi Mungu,

uovu wao nimeuona hata ndani ya nyumba yangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

12Kwa hiyo njia zao zitakuwa zenye utelezi na giza,

watajigonga na kuanguka;

maana, nitaleta hasara juu yao

mwaka wa kuwaazibu utakapotimia.

–Ni ujumbe wa Yawe.

13Kati ya manabii wa Samaria,

nimeona jambo la kuchukiza sana:

nao walitabiri kwa jina la mungu Bali

na kupotosha watu wangu Waisraeli.

14Lakini kati ya manabii wa Yerusalema,

nimeona mambo ya kutisha zaidi:

wao wanafanya uzinzi na kusema uongo;

wanawaunga mukono wanaotenda maovu

hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu.

Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma;

wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.

15Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya manabii wa Yerusalema:

Nitawakulisha uchungu,

na kuwapa maji yenye sumu wakunywe.

Maana kutoka kwa manabii wa Yerusalema

kutomwogopa Mungu kumeenea kila pahali katika inchi.

16Yawe wa majeshi anasema hivi: Musisikilize maneno manabii wanaowatabiria; wanawapa matumaini ya uongo. Yale wanayowaambia ni maono ya mioyo yao wenyewe. Hayakutoka katika kinywa cha Yawe.

17Wanawaambia hivi wale wanaozarau neno langu mimi Yawe: Mambo yenu yataendelea vizuri. Na wanamwambia hivi kila mutu anayefuata ugumu wa moyo wake na mawazo yake: Hakuna hasara yoyote itakayokupata!

18Lakini ni nani kati ya manabii hao

aliyehuzuria katika baraza la Yawe,

hata akasikia na kuelewa neno lake?

Au ni nani aliyejali neno lake,

hata akalielewa?

19Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe;

kasirani yake imeamuka,

upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.

20Hasira ya Yawe haitatulia,

mpaka atakapotimiza na kukamilisha

mapenzi ya moyo wake.

Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.

21Yawe anaendelea kusema:

Mimi sikuwatuma hao manabii,

lakini wao walikwenda mbio;

sikuwaambia kitu chochote,

lakini wao walitabiri!

22Kama wangalihuzuria katika baraza langu,

wangalitangazia watu wangu maneno yangu,

wangaliwageuza kutoka katika njia zao mbaya,

na kutoka katika matendo yao maovu.

23Mimi ni Mungu wa karibu, wala si Mungu wa mbali.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

24Mutu anaweza kujificha pahali pa siri hata nisiweze kumwona?

–Ni ujumbe wa Yawe!–

Hamujui kwamba niko kila pahali, katika mbingu na katika dunia?

–Ni ujumbe wa Yawe!–

25Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!

26Itakuwa hivyo mpaka wakati gani? Hao manabii wataendelea mpaka wakati gani kupotoka moyo, kutabiri uongo na udanganyifu wao wanaojitungia wenyewe?

27Kwa ndoto hizo zao wanafikiri kwamba watawashawishi watu wangu wanisahau mimi kama vile babu zao walivyonisahau, na kumufuata mungu Bali!

28Nabii aliyeota ndoto, atangaze ndoto yake, lakini yule aliyefunuliwa ujumbe wangu autangaze kwa uaminifu. Kuna ulinganifu gani kati ya maganda na ngano?

–Ni ujumbe wa Yawe.–

29Neno langu ni kama moto.

–Ni ujumbe wa Yawe!–

Neno langu ni kama nyundo inayovunja mawe vipandevipande.

30Kwa hiyo, mimi nitawashambulia manabii.

–Ni ujumbe wa Yawe!–

Wanadanganyana kwamba nimetoa ujumbe kwao.

31Kweli mimi nitawashambulia manabii.

–Ni ujumbe wa Yawe!

Wanajitungia maneno yao wenyewe na kusema “Ni ujumbe wa Yawe”.

32Vilevile mimi Yawe ninasema kwamba nitawashambulia manabii wanaotabiri ndoto zao za uongo kwa watu wangu, na kuwapotosha kwa uongo wao na upuuzi wao. Mimi sikuwatuma wala kuwaamuru waende, kwa hiyo hawatawafalia watu hao kitu.

–Ni ujumbe wa Yawe!

33Yawe akaniambia: Mutu yeyote, akuwe nabii au kuhani akikuuliza “Uko wapi muzigo Yawe anaotubebesha?”, wewe utawaambia: Ninyi ndio muzigo kwa Yawe, naye atawatupa mbali. –Ni ujumbe wa Yawe!–

34Tena nabii au kuhani, au mutu yeyote atakayesema: “Muzigo wa Yawe”, nitamwazibu pamoja na jamaa yake yote.

35Kitu munachopaswa kuulizana ninyi kwa ninyi ni hiki: “Yawe amejibu nini?” au, “Yawe amesema nini?”

36Lakini jambo la “Muzigo wa Yawe”, musilitaje tena. Neno mwanadamu analosema litakuwa muzigo kwake mwenyewe, kwa maana munageuza maneno yangu mimi Mungu Mwenye Uzima, Yawe wa majeshi, Mungu wenu.

37Basi mukiuliza neno kwa nabii, museme hivi: Yawe amekujibu nini? au, Yawe amesema nini?

38Lakini wao wakivunja amri yangu na kuendelea kusema Muzigo wa Yawe, wakati ambapo mimi niliwakataza wasiseme vile. Basi, uwaambie

39mimi nitawanyanyua na kuwatupilia mbali, wao wenyewe pamoja na muji niliowapa wao na babu zao.

40Nitawafanya wafezeheke hata milele na kupata haya ya kudumu ambayo haitasahaulika.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help