1Mufalme Adoni-Zedeki wa Yerusalema akapata habari juu ya jinsi Yoshua alivyouteka muji wa Ai na kuuharibu kabisa akiutendea muji huo na mufalme wake kama alivyoutendea Yeriko na mufalme wake. Vilevile akapata habari kwamba wakaaji wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli na kwamba sasa wanaishi kati yao.
2Habari hizo zilisababisha hofu kubwa kule Yerusalema kwa sababu muji wa Gibeoni ulikuwa mukubwa sana kati ya miji ya kifalme. Muji huu ulikuwa vilevile mukubwa kuliko Ai na wanaume wake wote walikuwa waaskari hodari sana.
3Basi, Mufalme Adoni-Zedeki akapeleka ujumbe kwa mufalme Hohamu wa Hebroni, mufalme Piramu wa Yarmuti, mufalme Yafia wa Lakisi na mufalme Debiri wa Eguloni, akawaambia:
4“Mukuje munisaidie tuwaangamize Wagibeoni, maana wamefanya mapatano ya amani na Yoshua pamoja na Waisraeli.”
5Kisha wafalme hao watano wa Waamori: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni, wakaunganisha waaskari wao, wakaenda nao mpaka Gibeoni. Wakapiga kambi kuuzunguka muji huo, wakaushambulia.
6Wagibeoni wakapeleka ujumbe kwa Yoshua kule katika kambi Gilgali, wakamwambia: “Tafazali, usitutupilie sisi watumishi wako. Ukuje mbio utusaidie na kutuokoa kwa maana wafalme wote wa Waamori kutoka inchi ya milima wamekuja kutushambulia.”
7Basi, Yoshua pamoja na jeshi lake lote na mashujaa wakaondoka Gilgali.
8Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”
9Nyuma ya kutembea kutoka Gilgali usiku kucha, Yoshua akawatokea kwa rafla.
10Naye Yawe akawatia hofu kubwa mbele ya Waisraeli ambao waliwaua watu wengi kule Gibeoni wakiwakimbia kwenye njia ya muteremuko wa Beti-Horoni mpaka Azeka na Makeda ambako vilevile waliwaua watu wengi sana.
11Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.
12Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema:
“Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni,
wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”
13Jua likasimama kimya na mwezi ukasimama mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi waadui zake. Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Yaseri, jua lilisimama kimya katikati ya mbingu, likakatiza safari yake ya kwenda kutua kwa siku nzima. Ang. 2 Sam 1.18
14Hakujakuwa siku kama hiyo hata kidogo wala haijapata kuonekana tena, siku ambayo Yawe amemwitikia mwanadamu kwa namna hiyo; maana Yawe mwenyewe aliwapigania Waisraeli.
15Kisha Yoshua akarudi katika kambi kule Gilgali pamoja na Waisraeli wote.
Yoshua anawaua wafalme watano wa Waamori16Wale wafalme watano wakakimbia na kujificha katika pango la Makeda.
17Yoshua akapata habari kwamba wafalme hao wamegunduliwa walikojificha katika pango la Makeda.
18Yoshua akasema: “Muviringishe mawe makubwa kwenye mulango wa pango na kuweka walinzi pale.
19Lakini ninyi musikae kule, muwafuatilie waadui zenu. Muwapige kutoka upande wa nyuma, wala musiwaache waingie katika miji yao, maana Yawe, Mungu wenu, amewatia katika mikono yenu.”
20Yoshua pamoja na Waisraeli wakawapiga na kuwaangamiza wote, na wachache wao walioponyoka wakakimbilia kwenye miji yao yenye kuta.
21Nyuma ya hayo Waisraeli wote wakarudi salama kwa Yoshua kule katika kambi Makeda; na hakuna tena mutu aliyesubutu kusema neno lolote juu ya Waisraeli.
22Kisha Yoshua akasema: “Mufungue mulango wa pango muniletee kutoka mule wale wafalme watano.”
23Wakafanya hivyo, wakamuletea Yoshua wale wafalme watano: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni.
24Wafalme hao walipoletwa, Yoshua akawaita Waisraeli wote na wakubwa wa waaskari waliokwenda naye kwa vita, akawaambia: “Mukuje karibu muwakanyage wafalme hawa kwenye shingo yao.” Nao wakasogea na kuwakanyaga kwenye shingo.
25Yoshua akawaambia: “Musiogope, wala musikuwe na wasiwasi, mukuwe imara na hodari, maana hivi ndivyo Yawe atakavyowatendea waadui zenu ambao mutapigana nao. Kwa hiyo, mukuwe imara na hodari.”
26Kisha, Yoshua aliwanyonga kwa kuwatundika kwenye miti mitano ambako walitundikwa mpaka magaribi.
27Wakati jua lilipokuwa karibu kutua, Yoshua aliamuru waondolewe juu ya miti walipokuwa wametundikwa na kutupwa katika pango walimokuwa wamejificha. Kisha wakaweka mawe makubwa kwenye mulango wa pango, nayo mawe hayo yako kule mpaka leo.
Yoshua anateka miji ya kusini28Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.
29Kutoka Makeda, Yoshua pamoja na Waisraeli wote walikwenda Libuna wakaushambulia.
30Yawe akautia muji huo pamoja na mufalme wao katika mikono ya Waisraeli, wakawaua wakaaji wake bila kuacha hata mutu mumoja. Walimutendea mufalme wa Libuna kama vile walivyomutendea mufalme wa Yeriko.
31Kisha kutoka Libuna Yoshua na Waisraeli wote walikwenda Lakisi, wakauzunguka muji ule na kuushambulia.
32Naye Yawe akautia muji huo katika mikono ya Waisraeli, wakauteka kisha siku mbili. Waliwaua wakaaji wote wa muji huo kama walivyofanya kule Libuna.
33Hapo, mufalme Horamu wa Gerezi akaamua kuja kuwasaidia watu wa Lakisi. Lakini Yoshua akamwua pamoja na watu wake wote, hakuacha hata mutu mumoja.
34Kisha kutoka Lakisi, Yoshua na Waisraeli wote walikwenda mpaka Eguloni, wakauzunguka muji ule na kuushambulia.
35Wakauteka siku hiyohiyo na kuwaua wakaaji wake wote kama walivyofanya kule Lakisi.
36Halafu kutoka Eguloni Yoshua na Waisraeli wote wakaenda mpaka Hebroni, wakaushambulia
37na kuuteka. Wakawaua wakaaji wake wote pamoja na mufalme wao; waliiharibu kabisa miji mingine iliyouzunguka, wakawaua wakaaji wake wote kama walivyofanya kule Eguloni.
38Kisha, Yoshua na Waisraeli wote wakarudi Debiri, wakaushambulia muji ule.
39Waliuteka muji huo na mufalme wake pamoja na miji mingine yote iliyouzunguka na kuwaangamiza wote waliokuwa ndani yao bila kuacha hata mutu mumoja. Waliutendea muji huo kama walivyoutendea muji wa Hebroni na muji wa Libuna na wafalme wao.
40Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.
41Yoshua akawashinda watu wote kutokea Kadesi-Barnea mpaka Gaza, na kutokea Goseni mpaka Gibeoni.
42Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.
43Basi, Yoshua akarudi mpaka katika kambi kule Gilgali pamoja na Waisraeli wote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.