1Haleluia!
Ee nafsi yangu, umusifu Yawe!
2Nitamusifu Yawe maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu muda wote nitakapoishi.
3Musiwategemee wakubwa wa dunia;
hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa.
4Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho,
anarudi katika mavumbi alimotoka,
na hapo mipango yake yote inatoweka.
5Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo,
mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,
6aliyeumba mbingu na dunia,
bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.
Yeye anashika ahadi yake milele.
7Yeye anawapatia wanaoonewa haki yao,
anawapa wenye njaa chakula.
Yawe anawapa wafungwa uhuru,
8anawafungua vipofu macho.
Yawe anawainua waliogandamizwa;
anawapenda watu wa haki.
9Yawe anawalinda wageni,
anawasaidia wajane na wayatima;
lakini anaharibu mipango ya waovu.
10Yawe anatawala milele.
Mungu wako, ee Sayuni, ni mufalme kwa vizazi vyote!
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.