1Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mutu mwovu kwa kuwa mushuhuda mubaya.
2Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.
3Usikuwe na upendeleo katika mashitaki ya masikini.
4Ukimukuta ngombe au punda wa adui yako amepotea, utamurudishia mwenye naye.
5Ukimwona punda wa mutu anayekuchukia ameanguka na muzigo wake, umusaidie mutu yule kumusimamisha punda wake, wala usimwache na kwenda zako.
6Usipotoshe haki masikini anayostahili katika mashitaki yake.
7Ujitenge mbali na mashitaki ya uongo wala usiwaue wasiokuwa na kosa na wenye haki, maana mimi sitamusamehe mutu mwovu.
8Usipokee kituliro, maana kituliro kinapofusha wakubwa na kupotosha mambo ya wenye haki.
9Usimutese mugeni. Ninyi munajua hali ya kuwa mugeni, maana mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.
Mwaka wa saba10Kwa muda wa miaka sita utapanda mashamba yako na kuvuna mazao yake.
11Lakini katika mwaka wa saba, utayaacha mashamba yako bila kupanda mbegu, kusudi wamasikini kati ya watu wako wapate chakula kilichobakia mule na nyama wa pori wakule. Utafanya vile vile katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12Kwa siku sita utafanya kazi zako, lakini siku ya saba utapumzika, kusudi ngombe wako na punda wako vilevile wapate kupumzika, na watoto wa mujakazi wako na wageni wapate kustarehe.
13Ushike mambo yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine, hayo yasisikilike katika kinywa chako.
Sikukuu tatu kubwa(Kut 34.18-26; Kumb 16.1-17)14Mara tatu kila mwaka mutafanya sikukuu kwa heshima yangu.
15Mutafanya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama vile nilivyowaagiza. Mutakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi ule mulitoka Misri. Mutu yeyote asikuje mbele yangu mikono mitupu.
16Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu. Ahadi na maagizo
20Muangalie, mimi ninamutuma malaika awatangulie katika safari kusudi awalinde na kuwafikisha katika inchi niliyowatayarishia.
21Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.
22Lakini mukimusikiliza kwa uaminifu na kufanya yote anayosema, mimi nitakuwa adui wa waadui zenu na mupinzani wa wapinzani wenu.
23Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika inchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanana, Wahivi na Wayebusi, nami nitawaangamiza wale wote.
24Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.
25Mutanitumikia mimi Yawe, Mungu wenu, nami nitawabariki kwa chakula na maji na kuondoa magonjwa kati yenu.
26Hakutakuwa mwanamuke yeyote atakayepoteza mimba wala kuwa tasa katika inchi yenu. Nami nitawajalia maisha marefu.
27Nitapeleka kitisho mbele yenu na kuwavuruga watu wote mutakaowafikia. Waadui zenu nitawafanya wageuke na kuwakimbia.
28Nitatuma nyuki mbele yenu ambazo zitawafukuza Wahivi, Wakanana na Wahiti.
29Sitawaondoa watu wale katika mwaka mumoja, inchi isibakie tupu na nyama wa pori wasiongezeke sana na kuwazidia nguvu.
30Lakini nitawaondoa kidogokidogo mpaka pale mutakapoongezeka na kurizi ile inchi.
31Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.
32Musifanye agano lolote nao, wala na miungu yao.
33Musiwaruhusu waishi katika inchi yenu wasiwasukume kutenda zambi mbele yangu. Maana kama mukitumikia miungu yao, hakika ile itakuwa mutego wa kuwanasa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.