Walawi 24 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Taa za Pahali Patakatifu(Kut 27.20-21)

1Yawe akamwambia Musa:

2Uwaamuru watu wa Israeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa kusudi taa hiyo iendelee kuwaka siku zote.

3Haruni ataweka taa hiyo ndani ya hema la mukutano, inje ya pazia la Sanduku la Agano kusudi ipate kuwaka mbele yangu tangu usiku mpaka asubui. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu.

4Ataweka hizo taa katika kinara cha taa cha zahabu safi ziwake siku zote mbele ya Yawe.

5Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili. Azabu ya haki

10Siku moja kukatokea fujo kule katika kambi kati ya Mwisraeli mumoja na kijana mumoja wa mama Mwisraeli lakini baba Mumisri.

11Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,

12wakamutia katika kifungo mpaka pale watakapofunuliwa mapenzi ya Yawe.

13Basi, Yawe akamwambia Musa:

14Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.

15Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote atakayemulaani Mungu wake atabeba lazima ya zambi yake.

16Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.

17Mutu yeyote anayeua mutu mwingine anapaswa naye kuuawa.

23Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help