Zaburi 70 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba musaada(Zab 40.13-17)

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea sadaka yake ya ukumbusho.

2Ee Mungu,

uniokoe!

Ee Yawe,

ukuje haraka unisaidie.

3Wapate haya na kufezeheka wanaotaka kuniua!

Warudi nyuma na kufezeheka wanaonitakia hasara!

4Wapumbazike kwa haya,

hao wanaofurahia kunizomea!

5Lakini wote wanaokutafuta,

wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.

Wote wanaopenda wokovu wako,

waseme siku zote: “Mungu ni mukubwa!”

6Nami ninayekuwa masikini na mukosefu,

unifikie haraka, ee Mungu!

Wewe ndiwe musaada wangu na mukombozi wangu.

Ee Yawe, usikawie!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help