Walawi 14 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Utakaso nyuma ya magonjwa ya ngoziSheria juu ya taka katika nguo

1Yawe akamwambia Musa:

2Hii ndiyo sheria juu ya mwenye ukoma katika siku ya kutakaswa kwake. Kisha kupona ataletwa kwa kuhani.

3Kuhani atakwenda kumwangalia yule mutu inje ya kambi. Ikiwa ukoma huo umepona,

4basi, kuhani ataamuru watu walete ndege wawili safi wanaokuwa wazima, kipande cha muti wa mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na tawi la hisopo kwa ajili ya yule mutu atakayetakaswa.

5Kuhani atawaamuru wachinje ndege mumoja katika chungu chenye maji safi ya chemichemi.

6Kuhani atatwaa yule ndege mwingine muzima, kipande kile cha mwerezi, sufu ya rangi nyekundu na lile tawi la hisopo na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa.

7Kisha, atamunyunyizia yule mwenye kutakaswa ile damu mara saba, halafu atamutangaza mutu huyo kuwa safi. Atamwacha yule ndege muzima aende zake katika pori inje ya muji.

8Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.

9Siku ya saba atanyoa nywele zake zote, ndevu na kope za macho yake. Kisha atafua nguo zake na kuoga, ataoga kwa maji, naye atakuwa safi.

10Siku ya nane ataleta wana-kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema, kondoo dike wa mwaka mumoja asiyekuwa na kilema, kilo tatu za unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula pamoja na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.

11Kuhani atakayetakasa mutu huyo atamuleta mbele ya Yawe karibu na mulango wa hema la mukutano pamoja na vitu alivyoleta.

12Kuhani atatwaa mwana-kondoo dume mumoja na kumutolea sadaka kwa ajili ya kosa pamoja na yale mafuta sehemu moja ya tatu ya litre. Atafanya kitambulisho cha kuvitolea mbele ya Yawe.

13Kisha atachinja yule mwana-kondoo katika Pahali Patakatifu, wanapochinjia nyama wa sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka hii kwa ajili ya kosa na vilevile sadaka kwa ajili ya zambi, ni mali ya kuhani. Ni sadaka takatifu kabisa.

14Kuhani atatwaa sehemu ya damu ya sadaka kwa ajili ya kosa na kumupakaa mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume na kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.

15Kisha, kuhani atatwaa sehemu ya ile sehemu moja ya tatu ya mafuta na kuyatia katika kigaja cha mukono wake wa kushoto.

16Atachovya kidole cha mukono wake wa kuume katika mafuta hayo na kumunyunyizia yule mutu anayetakaswa mara saba mbele ya Yawe.

17Sehemu ya mafuta yanayobaki katika kigaja chake ataipakaa mutu yule anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume na kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume, pahali palepale alipomupakaa damu ya sadaka kwa ajili ya kosa.

18Yale mafuta yaliyobaki atayapakaa yule mutu kwenye kichwa. Hivyo kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.

19Kuhani atatolea sadaka kwa ajili ya zambi na kumufanyia yule mutu anayetakaswa ibada ya upatanisho kwa kumwondolea uchafu wake. Kisha atachinja mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.

20Kuhani atatolea ile sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya vyakula juu ya mazabahu. Hivyo kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.

21Lakini ikiwa mutu yule ni masikini, hana uwezo wa kutoa vitu hivyo, basi ataleta mwana-kondoo dume mumoja kuwa malipo ya sadaka kwa ajili ya kosa ambaye atafanyiwa kitambulisho cha kutoa sadaka kwa kumufanyia yule mutu ibada ya upatanisho. Ataleta vilevile kilo moja ya unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula na mafuta sehemu moja ya tatu ya litre.

22Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.

23Siku ya nane atamuletea kuhani vitu hivyo mbele ya mulango wa hema la mukutano kwa ajili ya utakaso wake mbele ya Yawe.

24Kuhani atatwaa yule mwana-kondoo dume wa sadaka kwa ajili ya kosa pamoja na yale mafuta sehemu moja ya tatu ya litre na kufanya kitambulisho cha kuvitolea mbele ya Yawe.

25Atachinja yule mwana-kondoo dume wa sadaka kwa ajili ya kosa. Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kumupakaa yule mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume, katika kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.

26Kuhani atatia sehemu ya mafuta hayo katika kigaja cha mukono wake wa kushoto.

27Kisha atamunyunyizia yule mutu kwa kidole cha mukono wake wa kuume sehemu ya hayo mafuta yanayokuwa katika kigaja chake cha kushoto mara saba mbele ya Yawe.

28Kuhani atamupakaa yule mutu anayetakaswa mafuta katika incha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mukono wake wa kuume, na kidole gumba cha muguu wake wa kuume. Atamupakaa pahali pale ambapo alimupakaa ile damu ya sadaka kwa ajili ya kosa.

29Mafuta yanayobakia katika mukono wake atayapakaa yule mutu kwenye kichwa, kwa kumufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.

30Kisha kuhani atatwaa mumoja wa wale hua au njiwa wawili kadiri mutu yule anavyoweza kuleta.

31Hua atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Pamoja na hao, atatoa sadaka ya vyakula. Kuhani atamufanyia mutu yule ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.

32Hii ndiyo sheria juu ya mutu mwenye ukoma asiyeweza kutoa sadaka za kumutakasa.

Ukoma katika nyumba

33Yawe akamwambia Musa na Haruni:

34Mutakapoingia katika inchi ya Kanana ambayo ninawapa kuwa urizi wenu, nami nikifanya namna ya ukoma uote katika ukuta wa nyumba fulani katika inchi mutakayorizi,

35basi, mwenye nyumba hiyo anapaswa kumwambia kuhani kwamba namna ya taka la ukoma imeonekana katika nyumba yake.

36Kuhani ataamuru vitu vyote ndani ya nyumba hiyo viondoshwe mbele yeye mwenyewe hajaanza uchunguzi wa taka lile, visipate vyote kutangazwa kuwa vichafu. Kisha kuhani ataingia kwa kuiangalia nyumba hiyo.

37Atachunguza taka lile. Kama taka lile limeonekana juu ya ukuta na limesababisha madoa ya rangi ya kijani kibichi au nyekundu na kuonekana kuwa yamepenya ndani ya kuta,

38basi, kuhani atatoka inje kwenye mulango na kufunga nyumba hiyo kwa muda wa siku saba.

39Siku ya saba kuhani atarudi na kuangalia tena nyumba hiyo. Ikiwa taka lile limeenea katika kuta za nyumba hiyo,

40kuhani ataamuru mawe yanayokuwa kwenye sehemu zenye taka lile yaondolewe na kutupwa pahali pachafu inje ya muji.

41Lipu ya ndani ya nyumba hiyo itakwaruzwa na uchafu wake utatupwa pahali pachafu inje ya muji.

42Kisha watatwaa mawe mapya na kujenga pahali walipobomoa. Nao watapiga nyumba hiyo lipu upya.

43Ikiwa taka lile litatokea tena kisha kutoa mawe hayo na kukwaruza lipu na kuipiga lipu upya,

44inapasa kuhani akuje kuichunguza. Ikiwa taka limeenea katika nyumba hiyo, basi huo ni ukoma wenye kuteketeza, nyumba hiyo ni chafu.

45Nyumba hiyo inapaswa kubomolewa na mawe yake, miti yake na lipu vipelekwe pahali pachafu inje ya muji.

46Zaidi ya hayo, yeyote atakayeingia ndani ya nyumba hiyo wakati itakapokuwa imefungwa, atakuwa muchafu mpaka magaribi.

47Yeyote anayelala katika nyumba hiyo au kukulia chakula ndani yake, anapaswa kufua nguo zake.

48Lakini ikiwa kisha kuchunguza nyumba hiyo, kuhani akiona kwamba taka halikuenea kisha kupigwa lipu, basi, kuhani atatangaza kwamba nyumba hiyo ni safi maana taka limekwisha.

49Kwa kutakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili pamoja na kipande cha muti wa mwerezi, sufu nyekundu na tawi la hisopo.

50Atachinja ndege mumoja katika chungu chenye maji safi ya chemichemi.

51Atatwaa kipande cha mwerezi, tawi la hisopo na ile sufu nyekundu pamoja na yule ndege mwingine anayekuwa muzima na kuvitumbukiza vyote katika damu ya yule ndege aliyechinjwa. Kisha atanyunyizia nyumba hiyo damu mara saba.

52Hivi ndivyo atakavyotakasa nyumba hiyo kwa damu ya ndege, maji safi ya chemichemi, ndege muzima, kipande cha muti wa mwerezi, tawi la hisopo na ile sufu nyekundu.

53Yule ndege anayekuwa muzima atamwacha aende zake katika pori inje ya muji. Hivi ndivyo atakavyotakasa nyumba hiyo, nayo itakuwa safi.

54Hii ndiyo sheria juu ya aina yoyote ya taka la ukoma;

55taka katika nguo au nyumba,

56kivimba, jipu au chunuku,

57kwa kuonyesha ni kitu gani kinachokuwa kichafu na kisichokuwa kichafu. Hiyo ndiyo sheria juu ya taka la ukoma.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help