1Mukuje tumwimbie Yawe,
tumushangilie yeye kikingio na mwokozi wetu!
2Tuende mbele yake na nyimbo za shukrani;
tumushangilie kwa nyimbo za sifa.
3Maana Yawe ni Mungu mukubwa;
yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote.
4Mabonde ni katika mikono yake,
vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;
kwa mikono yake aliumba inchi kavu.
6Mukuje tuiname chini na kumwabudu;
tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!
7Maana yeye ni Mungu wetu.
Sisi ni watu wake,
kondoo wanaochungwa katika malisho yake.
Heri leo mungesikiliza hivi anavyosema:
8“Musikuwe wagumu kama kule Meriba,
kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,
9babu zenu waliponijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
10Kwa miaka makumi ine nilichukizwa nao,
nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!
Hawajali kabisa njia zangu!’
11Basi, nikaapa kwa kasirani kwamba
hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.