Zaburi 95 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wimbo wa kumusifu Mungu

1Mukuje tumwimbie Yawe,

tumushangilie yeye kikingio na mwokozi wetu!

2Tuende mbele yake na nyimbo za shukrani;

tumushangilie kwa nyimbo za sifa.

3Maana Yawe ni Mungu mukubwa;

yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote.

4Mabonde ni katika mikono yake,

vilele vya milima ni vyake.

5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;

kwa mikono yake aliumba inchi kavu.

6Mukuje tuiname chini na kumwabudu;

tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!

7Maana yeye ni Mungu wetu.

Sisi ni watu wake,

kondoo wanaochungwa katika malisho yake.

Heri leo mungesikiliza hivi anavyosema:

8“Musikuwe wagumu kama kule Meriba,

kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa,

9babu zenu waliponijaribu na kunipima,

ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.

10Kwa miaka makumi ine nilichukizwa nao,

nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!

Hawajali kabisa njia zangu!’

11Basi, nikaapa kwa kasirani kwamba

hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help