Ezekieli 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufano wa muzabibu

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

2Wewe mwanadamu! Muti wa muzabibu ni bora kuliko miti mingine ya pori?

3Muti wake unafaa kwa kutengeneza kitu chochote? Watu wanaweza kuutumia kwa kutengeneza misumari ya kutundika vitu?

4Huo unafaa tu kwa kukonga moto. Tena moto unapoteketeza sehemu yake ya mwanzo na ya mwisho na kuikausha sehemu ya katikati, hiyo inafaa kwa kitu chochote?

5Ulipokuwa haujachomwa ulikuwa haufai kitu, kefu sasa unapokwisha kuchomwa kwa moto na kuwa makaa! Haufai kitu kabisa.

6Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile nilivyoutoa muti wa muzabibu kati ya miti ya pori kuwa kuni za kukonga moto, ndivyo nilivyotoa wakaaji wa Yerusalema.

7Nitawaazibu vikali. Hata kama wataukimbia moto, huo moto utawateketeza. Hapo nitakapowaazibu vikali, halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.

8Kwa sababu wamekosa uaminifu kwangu, nitaifanya inchi yao kuwa ukiwa.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help