1Haleluia!
Mumusifu Yawe kutoka mbinguni,
mumusifu kutoka huko juu mbinguni.
2Mumusifu enyi wamalaika wake wote,
mumusifu enyi jeshi lake lote.
3Mumusifu enyi jua na mwezi,
mumusifu enyi nyota zote zinazoangaza.
4Mumusifu enyi mbingu za juu,
na maji yanayokuwa juu ya mbingu.
5Vyote visifu jina la Yawe,
maana yeye aliamuru, na vyote vikakuwa.
6Yeye aliviweka nafasi yao kwa milele,
kwa amri ambayo haiwezi kuvunjika.
7Mumusifu Yawe tokea katika dunia;
enyi nyoka wakubwa wa bahari na mashimo ya bahari, mumusifu.
8Mumusifu, enyi moto, mvua ya mawe na teluji,
upepo wenye zoruba unaotimiza amri yake!
9Mumusifu, enyi milima na vilima,
miti ya matunda na ya mierezi!
10Mumusifu, enyi nyama wa pori na wa kufugwa,
viumbe vinavyotambaa na ndege wote!
11Mumusifu, enyi wafalme na mataifa yote;
waongozi na watawala wote katika dunia!
12Mumusifu, enyi vijana wanaume na wabinti;
wazee wote na watoto!
13Wote musifu jina la Yawe,
maana jina lake peke yake linatukuzwa;
utukufu wake unapita dunia na mbingu.
14Amewapa watu wake nguvu;
nayo heshima kwa watu wote waaminifu,
ndio watu wa Israeli wapendwa wake.
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.