ZAKARIA 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hukumu juu ya mataifa jirani

1Ujumbe wa Yawe:

Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki.

Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe,

kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,

2vilevile muji wa Hamati unaopakana na Hadiraki,

na hata miji ya Tiro na Sidona

ingawa inajiona kuwa na hekima sana.

3Muji wa Tiro umejijengea kuta kubwa,

umejilundikia feza kama mavumbi,

na zahabu kama takataka katika barabara.

4Lakini Bwana atatwaa mali yake yote,

atautumbukiza utajiri wake katika bahari,

na kuuteketeza muji ule kwa moto.

5Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa,

nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu;

hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka.

Gaza utapoteza mufalme wake,

nao Askeloni hautakaliwa na watu.

6Muji wa Asidodi utakaliwa na wana haramu.

Yawe anasema hivi:

Nitakikomesha kiburi cha Wafilistini.

7Nitawakomesha kula nyama yenye damu,

na chakula ambacho ni chukizo.

Watakaobaki watakuwa mali yangu,

kama ukoo mumoja katika Yuda.

Watu wa Ekroni watakuwa kama Wayebusi.

8Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu,

nitazuia majeshi yasipitepite ndani.

Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu,

maana, kwa macho yangu mwenyewe,

nimeona jinsi walivyoteseka.

Mufalme wa amani

9Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni!

Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema!

Angalia, mufalme wenu anawakujia,

anakuja kwa shangwe na ushindi!

Ni mupole, amepanda juu ya punda,

juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.

10Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu,

na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema;

pinde za vita zitatupwa mbali.

Naye ataleta amani kati ya mataifa;

utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari,

toka muto Furati hata miisho ya dunia.

Kurudishwa kwa watu wa Mungu

11Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya agano langu pamoja nanyi,

agano lililokamilishwa kwa njia ya damu,

nitawakomboa wafungwa wenu

wanaokuwa kama wamefungwa katika shimo tupu.

12Enyi wafungwa wenye tumaini,

murudi kwenye ukuta wa muji wenu.

Sasa mimi ninawatangazia:

nitawarudishia mema mara mbili.

13Yuda nitamutumia kama upinde wangu;

Efuraimu nimemufanya mushale wangu.

Ee Sayuni, watu wako nitawatumia kama upanga

kwa kuwashambulia watu wa Ugriki;

watakuwa kama upanga wa shujaa.

14Yawe atawatokea watu wake;

atafyatua mishale yake kama umeme.

Bwana wetu Yawe atapiga baragumu;

atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.

15Yawe wa majeshi atawalinda watu wake,

nao watawaangamiza waadui zao.

Watapiga kelele katika vita kama walevi,

wataimwanga damu ya waadui zao.

Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka

iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.

16Wakati ule, Yawe, Mungu wao, atawaokoa,

maana wao ni kundi lake;

nao watangaa katika inchi yake

kama mawe ya bei kali katika taji.

17Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa!

Vijana wanaume na wanawake watastawi

kwa wingi wa ngano na divai mupya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help