1Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.
2Yawe, Mungu wetu, alifanya agano nasi kwenye mulima Horebu.
3Hakufanya agano hilo na wazee wetu, lakini alilifanya na sisi wote ambao tuko wazima hivi leo.
4Yawe alisema nanyi kinywa kwa kinywa huko kwenye mulima katikati ya moto.
5Wakati huo mimi nikasimama kati yenu na Yawe, nikawatangazia yale aliyosema, kwa sababu ninyi muliogopa ule moto na hamukupanda juu ya mulima.
Yawe akasema hivi:
6“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.
7“Usikuwe na miungu mingine isipokuwa mimi.
8“Usijifanyie sanamu za miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.
9Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.
10Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.
11“Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.
12“Shika siku ya Sabato na kuitakasa, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru.
13Siku sita fanya kazi na tenda mambo yako yote.
14Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala ngombe wako, wala punda wako, wala nyama wako yeyote, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako, kusudi mutumwa wako na mujakazi wako wapate kupumzika vilevile kama vile wewe.
15Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.
16“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.
17“Usiue.
18“Usizini.
19“Usiibe.
20“Usimushuhudie mwenzako uongo.
21“Usimutamani muke wa mwenzako, wala nyumba yake, wala shamba lake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.”
Musa musemaji wa Mungu(Kut 20.18-21)22“Hizi ndizo amri Yawe alizowaambia ninyi wote kwa sauti kubwa kutoka katika moto na lile wingu zito na giza nene, mulipokuwa mumekusanyika kule kwenye mulima. Hakuongeza hapo amri ingine. Kisha akaandika juu ya vibao viwili vya mawe, akanipatia.
23“Wakati muliposikia hiyo sauti kutoka katikati ya lile giza, juu ya ule mulima uliokuwa unawaka moto, viongozi wote wa makabila yenu na wazee walinifikia
24wakasema: ‘Sikiliza! Yawe, Mungu wetu, ametufunulia utukufu na ukubwa wake. Tumeisikia sauti yake kutoka katikati ya ule moto. Leo hivi tumemwona Mungu akisema na mwanadamu, naye mwanadamu pahali pa kufa akaendelea kuishi!
25Lakini kwa nini kujitia katika hatari ya kufa kwa kuteketezwa na ule moto mukubwa? Tukisikia tena sauti ya Yawe, Mungu wetu tutakufa!
26Ni mwanadamu gani aliyepata kusikia sauti ya Mungu Mwenye Uzima kutoka katikati ya moto kama vile tulivyomusikia sisi halafu akaweza kubaki muzima?
27Heri wewe Musa uende karibu, usikilize yote Yawe, Mungu wetu, atakayosema, kisha ukuje kutuambia mambo hayo yote atakayokuambia. Sisi tutayasikiliza na kuyatimiza’.
28“Bwana akasikia hayo maneno yenu, akaniambia: ‘Nimesikia maneno watu hawa waliyokuambia. Yote waliyosema ni sawa.
29Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.
30Kwenda uwaambie warudi ndani ya mahema yao.
31Lakini wewe Musa usimame hapa karibu nami. Mimi nitakuambia amri zote na masharti na maagizo ambayo utawafundisha, kusudi inchi ambayo ninawapa ikuwe mali yao.’
32“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.
33Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.