Zaburi 112 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Furaha ya mutu mwema

1Haleluia!

Heri mutu anayemuheshimu Yawe,

anayefurahia sana kushika amri zake.

2Wazao wake watakuwa wenye nguvu katika inchi;

watoto wa watu wa usawa watapata baraka.

3Ndani ya nyumba yake kutakuwa mali nyingi;

haki yake utadumu milele.

4Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza;

yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.

5Mutu muzuri anakopesha bila faida;

anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.

6Hatashindwa hata kidogo;

atakumbukwa milele.

7Haogopi habari mbaya;

moyo wake unasimama imara na anamutegemea Yawe.

8Yuko imara ndani ya moyo, wala hataogopa;

naye ataona waadui zake wakishindwa.

9Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini.

Haki yake inadumu milele.

Ana nguvu na sifa.

10Watu waovu wanaona hayo na kuuzika.

Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka.

Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help