1Viongozi wa jamaa katika ukoo wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase mwana wa Yosefu, wakakwenda kuzungumuza na Musa na viongozi wengine wa ukoo za Waisraeli.
2Wakasema: Yawe alikuamuru kuwagawanyia watu wa Israeli inchi kwa kura kuwa urizi wao; alikuamuru vilevile uwape wabinti za Selofehadi ndugu yetu urizi wa baba yao. wamesema ukweli.
6Na hivi ndivyo Yawe anavyoamuru juu ya wabinti za Selofehadi; wako huru kuolewa na mutu yeyote wanayemupenda, lakini waolewe katika kabila lao,
7kusudi urizi wa Waisraeli usihamishiwe kwa kabila lingine; kila Mwisraeli atabakia na urizi wa kabila lake.
8Mwanamuke yeyote mwenye urizi katika kabila moja la Israeli anapaswa kuolewa na mutu wa kabila lake, kusudi kila Mwisraeli abakie na urizi wa babu zake.
9Hivyo hakutakuwa urizi wowote utakaohamishwa kutoka kabila moja kwa lingine. Kila kabila la Waisraeli litashikilia urizi wake.
10Wabinti za Selofehadi wakafanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
11Wote: Mala, Tirsa, Hogla, Milka na Noa wakaolewa na binamu zao.
12Wakaolewa katika jamaa za ukoo wa Manase mwana wa Yosefu, na urizi wao ukabaki katika kabila la baba yao.
13Hizo ndizo amri na maagizo ambayo Yawe aliwapa Waisraeli kwa njia ya Musa katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na muji wa Yeriko.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.