1Kisha katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili nyuma ya Waisraeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa katika jangwa la Sinai. Akamwambia:
2Waisraeli washike sikukuu ya Pasaka kwa wakati uliopangwa.
3Hii itakuwa siku ya kumi na ine ya mwezi huu, wakati wa magaribi watafanya hivyo kufuatana na masharti na maagizo yake yote.
4Kwa hiyo, Musa akawaambia watu kwamba wanapaswa kushika sikukuu ya Pasaka.
5Basi, wakafanya Pasaka magaribi, siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, katika jangwa la Sinai. Waisraeli wakafanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
6Lakini, watu wamoja waliokuwa pale walikuwa hawawezi kushiriki sikukuu hiyo ya Pasaka kwa sababu walikuwa wamegusa maiti, wakakuwa wachafu. Hao waliwaendea Musa na Haruni,
7wakawaambia: Sisi tuko wachafu kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tukatazwe kumutolea Yawe sadaka zake kwa wakati uliopangwa pamoja na Waisraeli wengine?
8Musa akawajibu: Mungojee mpaka pale nitakapopata maagizo juu yenu kutoka kwa Yawe.
9Naye Yawe akamwambia Musa:
10Mumoja wenu au mumoja wa wazao wenu akiwa muchafu kwa sababu amegusa maiti au akiwa mbali katika safari, lakini akiwa anataka kunifanyizia sikukuu ya Pasaka,
11mutu kama huyo anaruhusiwa kufanya hivyo mwezi mumoja kisha, magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa pili. Ataifanya kwa kula mikate isiyotiwa chachu na mboga chungu.
12Wasiache chakula chochote mpaka asubui, wala wasivunje hata mufupa mumoja wa nyama wa Pasaka. Watafanya sikukuu hii ya Pasaka kulingana na sharti lake lote.
13Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.
14Ikiwa kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi na anapenda kufanya sikukuu ya Pasaka, mutu huyo sharti afanye hivyo kulingana na masharti na maagizo yote ya Pasaka. Kila mutu atafuata masharti yaleyale, akiwa mugeni au mwenyeji.
Wingu la moto(Kut 40.34-38)15Siku ambayo hema takatifu lilisimikwa, wingu likashuka na kufunika hema la kuchunga vibao vya agano. Wakati wa usiku wingu hilo lilionekana kama moto mpaka asubui.
16Hivi ndivyo ilivyokuwa kila siku; wingu lilifunika hema muchana, na usiku lilionekana kama moto.
17Kila mara wingu hilo lilipoinuliwa juu ya hema, Waisraeli walivunja kambi na kupiga kambi tena pahali wingu hilo lilipotua.
18Walisafiri kwa amri ya Yawe, na kupiga kambi tena kwa amri yake. Muda wote wingu hilo lilipokuwa juu ya hema, watu walikaa katika kambi hiyo.
19Hata kama wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku nyingi, Waisraeli walimutii Yawe, nao hawakuondoka.
20Wakati mwingine wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku chache tu. Kwa agizo la Yawe, Waisraeli walipiga kambi na ni kwa agizo la Yawe walisafiri.
21Wakati mwingine wingu lilikaa juu ya hema tangu magaribi mpaka asubui tu; na mara tu lilipoinuliwa, hao watu vilevile walifunga safari. Na ikiwa lilikaa juu ya hema muchana kutwa na usiku kucha, wao waliondoka tu wingu lilipoinuliwa.
22Ikiwa ni siku mbili, mwezi, mwaka au zaidi, muda wote wingu hilo lilipokuwa juu ya hema, Waisraeli hawakuhama; lakini lilipoinuliwa, nao vilevile walihama.
23Kwa agizo la Yawe walipiga kambi na kwa agizo la Yawe walisafiri. Walishika agizo la Yawe kama vile alivyotoa amri yake kwa njia ya Musa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.