1Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake.
2Viongozi wao walikuwa Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Seraya, Relaya, Mordekayi, Bilsani, Misipari, Bigwayi, Rehumu na Bana.
Hii ndiyo hesabu ya watu wote wa ukoo za Waisraeli waliorudi kutoka katika uhamisho:
3wa ukoo wa Parosi: elfu mbili mia moja makumi saba na wawili;
4wa ukoo wa Sefatia: mia tatu makumi saba na wawili;
5wa ukoo wa Ara: mia saba makumi saba na watano;
6wa ukoo wa Pahati-Moabu, maana yake wazao wa Yesua na Yoabu: elfu mbili mia nane kumi na wawili;
7wa ukoo wa Elamu: elfu moja mia mbili makumi tano na wane;
8wa ukoo wa Zatu: mia tisa makumi ine na watano;
9wa ukoo wa Zakayi: mia saba na makumi sita;
10wa ukoo wa Bani: mia sita makumi ine na wawili;
11wa ukoo wa Bebayi: mia sita makumi mbili na watatu;
12wa ukoo wa Azgadi: elfu moja mia mbili makumi mbili na wawili;
13wa ukoo wa Adonikamu: mia sita makumi sita na sita;
14wa ukoo wa Bigwayi: elfu mbili na makumi tano na sita;
15wa ukoo wa Adini: mia ine makumi tano na wane,
16wa ukoo wa Ateri, ndiye Hezekia: makumi kenda na wanane;
17wa ukoo wa Besayi: mia tatu makumi mbili na watatu;
18wa ukoo wa Yora: mia moja kumi na wawili;
19wa ukoo wa Hasumu: mia mbili makumi mbili na watatu;
20wa ukoo wa Gibari: makumi kenda na watano.
21Watu wa muji wa Betelehemu: mia moja makumi mbili na watatu;
22wa muji wa Netofa: makumi tano na sita;
23wa muji wa Anatoti: mia moja makumi mbili na wanane;
24wa muji wa Azimaweti: makumi ine na wawili;
25wa muji wa Kiriati-Yearimu, wa Kefira na wa Beroti: mia saba makumi ine na watatu;
26wa muji wa Rama na wa Geba: mia sita makumi mbili na mumoja;
27wa muji wa Mikimasi: mia moja makumi mbili na wawili;
28wa muji wa Beteli na Ai: mia mbili makumi mbili na watatu;
29wa muji wa Nebo: makumi tano na wawili;
30wa muji wa Magibisi: mia moja makumi tano na sita;
31wa muji wa Elamu wa pili: elfu moja mia mbili makumi tano na wane;
32wa muji wa Harimu: mia tatu na makumi mbili;
33wa muji wa Lodi, Hadidi na wa Ono: mia saba makumi mbili na watano;
34wa muji wa Yeriko: mia tatu makumi ine na watano;
35wa muji wa Sena: elfu tatu mia sita na makumi tatu.
36Hii ndiyo jumla ya makuhani waliorudi kutoka katika uhamisho:
wa ukoo wa Yedaya waliokuwa wazao wa Yesua: mia tisa makumi saba na watatu;
37wa ukoo wa Imeri: elfu moja na makumi tano na wawili;
38wa ukoo wa Pashuri: elfu moja mia mbili makumi ine na saba;
39wa ukoo wa Harimu: elfu moja na kumi na saba.
40Walawi wa ukoo wa Yesua na wa Kadimieli, wazao wa Hodavia waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa makumi saba na wane.
41Waimbaji (wazao wa Asafu), walikuwa mia moja makumi mbili na wanane.
42Walinzi wa mulango (wazao wa Salumu, wa Ateri, wa Talmoni, wa Akubu, wa Hatita na wa Sobayi), walikuwa mia moja makumi tatu na tisa.
43-54Hizi ni ukoo za watumishi wa hekalu waliorudi kutoka katika uhamisho:
Siha, Hasufa, Tabaoti,
Kerosi, Siaha, Padoni,
Lebana, Hagaba, Akubu,
Hagabu, Semaya, Hanani,
Gideli, Gahari, Raya,
Resini, Nekoda, Gazamu,
Uza, Pasea, Besayi,
Asina, Munimu, Nefisimu,
Bakuki, Hakufa, Harihuri,
Basiluti, Mehida, Harsa,
Barkosi, Sisera, Tema,
Nezia, Hatifa.
55-57Kati ya wazao wa watumishi wa Solomono, waliorudi kutoka katika uhamisho, kulikuwa wazao wa watu hawa:
Sotayi, Hasofereti, Peruda,
Yala, Darkoni, Gideli,
Sefatia, Hatili,
Pokereti-Hazebaimu, Ami.
58Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Solomono waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa watu mia tatu makumi kenda na wawili.
59Watu walirudi kutoka miji hii: Teli-Mela, Teli-Harsa, Kerubu, Adani na Imeri. Lakini hawakuweza kuhakikisha kwamba walikuwa wazao wa Waisraeli.
60Wao walikuwa watu wa ukoo wa Delaya wa Tobia na wa Nekoda, kwa jumla watu mia sita makumi tano na wawili.
61Watu wa ukoo hizi za makuhani vilevile walirudi: ukoo wa Habaya, wa Hakosi na wa Barzilayi. Huyo Barzilayi alikuwa ameoa binti ya Barzilayi wa Gileadi, naye vilevile akaitwa Barzilayi.
62Hao walitafuta ukoo wao katika kitabu cha ukoo, lakini hawakuonekana humo. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kushika ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu.
63Mutawala akawaambia kwamba hawaruhusiwi kushiriki chakula kitakatifu sana, mpaka kukuwe kuhani atakayeweza kutoa shauri kwa njia Urimu na Tumimu.
64-67Hii ni jumla ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho, pamoja na watumishi na nyama wao:
Waisraeli: elfu makumi ine na mbili, mia tatu na makumi sita.
Watumishi wanaume na wanawake: elfu saba mia tatu makumi tatu na saba.
Waimbaji wanaume na wanawake: mia mbili.
Farasi: mia saba makumi tatu na sita.
Nyumbu: mia mbili makumi ine na watano.
Ngamia: mia ine makumi tatu na watano.
Punda: elfu sita mia saba na makumi mbili.
68Watu hao waliotoka katika uhamisho, walipofika kwenye nyumba ya Yawe katika Yerusalema, viongozi wamoja wa ukoo hizo walitoa matoleo ya mapenzi kwa kusaidia ujenzi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema.
69Walitoa kila mutu kadiri ya uwezo wake kwa ajili ya kazi hii. Jumla ya matoleo hayo ilikuwa kilo mia tano za zahabu, kilo elfu mbili na mia nane za feza na nguo mia moja kwa ajili ya makuhani.
70Basi, makuhani, Walawi na watu wengine wamoja wakaanza kuishi katika Yerusalema na katika vijiji vyake. Nao waimbaji, walinzi wa hekalu na watumishi wa hekalu wakaanza kuishi katika miji yao; Waisraeli wote wakaishi katika miji yao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.