1Musa akaendelea kusema na Waisraeli wote,
2akawaambia: “Mimi sasa nina umri wa miaka mia moja na makumi mbili, na sina nguvu ya kufanya kazi zaidi. Tena Yawe ameniambia kwamba sitavuka muto Yordani.
3Yawe, Mungu wenu, atawatangulia na kuyaangamiza mataifa yanayoishi huko, kusudi murizi inchi yao. Yoshua atakuwa kiongozi wenu kama vile Yawe alivyosema.
4Yawe atayaangamiza mataifa hayo kama vile alivyowaangamiza Sihoni na Ogi, wafalme wa Waamori, na inchi yao.
5Yawe atawapa ushindi juu yao nanyi mutawatendea kama vile nilivyowaamuru.
6Mukuwe imara na hodari, wala musiwaogope au kutishwa nao, maana Yawe, Mungu wenu, ndiye anayekwenda pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa.”
7Kisha Musa akamwita Yoshua, akamwambia mbele ya watu wote wa Israeli: “Ukuwe imara na hodari, maana wewe utawaongoza watu hawa kwenda kurizi inchi ambayo Yawe aliwaahidi babu zao, nawe utawapatia wairizi.
8Yawe ndiye anayewaongoza. Yeye atakuwa pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa. Hivyo, musiogope wala musifazaike.”
Kukumbuka sheria kila mwaka wa saba9Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.
10Kisha akawaamuru akasema: “Kila mwaka wa saba utakuwa mwaka wa mafungulio. Katika sikukuu ya vibanda, mwaka huo,
11wakati watu wa Israeli wanapokuja mbele ya Yawe pahali pale atakapochagua, mutawasomea watu wote wa Israeli sheria hii.
12Mutakusanya wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, kusudi kila mumoja asikie maneno haya ya kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kuwa waangalifu kushika maneno ya sheria hii.
13Nao wazao wao ambao hawajasikia sheria ya Yawe, Mungu wenu, wapate kuisikia na kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, muda wote mutakaoishi katika inchi ambayo munakwenda kurizi ngambo ya muto Yordani.”
14Yawe akamwambia Musa: “Siku yako ya kuaga dunia imekaribia. Umwite Yoshua, mukuje pamoja katika hema la mukutano kusudi nimupe maagizo.” Basi, Musa na Yoshua wakaenda katika hema la mukutano,
15naye Yawe akawatokea humo katika nguzo ya wingu ambayo ilisimama kwenye mulango wa hema.
16Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.
17Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.
18Hakika nitawaficha uso wangu kwa sababu wamefanya mambo maovu na kugeukia miungu mingine.
19“Sasa, andika wimbo huu, uwafundishe watu wa Israeli kusudi ukuwe ushuhuda wangu juu yao.
20Nitakapowapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali, kama vile nilivyowaapia babu zao, nao watakula, watashiba na kunenepa, halafu watageukia miungu mingine na kuitumikia. Watanizarau na kuvunja agano langu.
21Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”
22Basi, Musa akaandika wimbo huo siku hiyohiyo, akawafundisha Waisraeli.
23Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”
24Musa alipomaliza kuandika maneno ya sheria hiyo tangu mwanzo mpaka mwisho,
25akawaambia Walawi waliokuwa wanabeba lile Sanduku la Agano la Yawe:
26“Mutwae kitabu hiki cha sheria, mukiweke karibu na Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, kusudi kikuwe ushuhuda juu yenu.
27Maana ninajua jinsi munavyokuwa waasi na wagumu. Ikiwa mumemwasi Yawe wakati niko muzima pamoja nanyi, itakuwa namna gani nyuma ya kifo changu?
28Uwakusanye mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na wakubwa wenu nipate kusema maneno haya wasikie, nayo dunia ishuhudie juu yao.
29Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”
Wimbo wa Musa30Halafu, Musa akasema maneno ya wimbo huu mbele ya kusanyiko lote la Waisraeli.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.