Hosea 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Hosea anatangaza azabu ya Israeli

1Musifurahi enyi Waisraeli!

Musishangilie kama watu wa mataifa mengine;

maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu.

Mumefurahia malipo ya uzinzi,

kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.

2Hawatapata chakula kutoka kiwanja cha kupepetea,

hawatapata divai mupya kutoka kikamulio.

3Hawatakaa katika inchi ya Yawe.

Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri.

Watakula vyakula vichafu kule Asuria.

4Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai,

wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao.

Chakula chao kitakuwa kama cha kilio,

wote watakaokikula watajichafua.

Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu,

hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.

5Mutafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa,

au katika karamu ya Yawe?

6Mutakapoyakimbia maangamizi ya inchi yenu,

Misri itawakaribisha ninyi kwake,

lakini makaburi yenu yanawangoja kule Memufisi.

Michongoma itaota katika vyombo vyenu vya feza,

miiba itajaa katika mahema yenu.

7Siku za azabu zimetimia,

siku za kulipiza kisasi zimefika;

Waisraeli lazima wautambue wakati huo!

Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu;

anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu.

Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa,

kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.

8Nabii ni mulinzi wa Waefuraimu kwa pahali pa Mungu;

lakini, popote anapoenda anategewa mutego kama ndege.

Hata katika nyumba ya Mungu wake anachukiwa.

9Ninyi mumezama katika uovu,

kama ilivyokuwa kule Gibea.

Mungu atayakumbuka makosa yao,

na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao. Zambi ya Israeli na matokeo yake

10Yawe anasema:

Nilipowakuta Waisraeli

walikuwa kama zabibu katika jangwa.

Nilipowaona babu zenu,

walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza.

Lakini walipofika kule Bali-Peori,

wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali,

wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.

11Utukufu wa Efuraimu utatoweka kama ndege;

watoto hawatazaliwa tena,

hakutakuwa watoto wa kuzaliwa,

wala hakutakuwa atakayepata mimba!

12Hata kama wakilea watoto,

sitamwacha hata mumoja wao muzima.

Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!

13Zamani, niliona kwamba

Efuraimu ilikuwa kama muti wa ngazi muchanga kwenye nafasi nzuri.

Lakini sasa Efuraimu italazimishwa kuwapeleka watoto wake wauawe.

14Uwaazibu watu hawa, ee Yawe!

Lakini utawaazibu namna gani?

Uwafanye wanawake wao kuwa tasa;

uwafanye wakose maziwa ya kunyonyesha watoto wao!

Hukumu ya Yawe kwa Israeli

15Yawe anasema hivi:

Uovu wao wote ulianzia Gilgali;

kule ndiko nilipoanza kuwachukia.

Kwa sababu ya uovu wa matendo yao,

nitawafukuza toka katika nyumba yangu.

Sitawapenda tena.

Wakubwa wao wote ni waasi.

16Watu wa Efuraimu wamepigwa,

wamekuwa kama muti wenye muzizi wenye kukauka,

hawatazaa watoto wowote.

Hata kama wakizaa watoto,

nitawaua watoto wao wanaowapenda.

17Kwa vile wamekataa kumusikiliza,

Mungu wangu atawatupilia;

wao watatangatanga kati ya mataifa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help